Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Jokate, Murro, Kafulila kumsaidia Rais Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Jokate, Murro, Kafulila kumsaidia Rais Magufuli

Spread the love

RAIS John Magufuli amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali, ambapo amemteua Mwanamitindo, Jokate Mwegelo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe huku aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila akimteua kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Songwe. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Rais Magufuli amefanya uteuzi huo leo tarehe 28 Julai, 2018 na Ikulu jijini Dar es Salaam.

Wengine walioteuliwa ni pamoja na Jerry Muro aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru wakati Patrobas Katambi akiteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma.

Vile vile, Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, ambapo Godfrey Chongolo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido akimteua kuirithi mikoba ya Hapi Kinondoni.

Na Lengay Ole Sabaya ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai. Pia, Rais Magufuli amemteua Moses Machali kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu.

Hapa chini orodha kamili ya mabadiliko yaliyofanywa na Rais Magufuli

Katibu tawala

Abubakar Musa – Dar es Salaam
David Kafulila – Songwe
Denis Bandisa – Geita
Happy William – Iringa
Abdallah Malela – Katavi
Rashid Chatta – Kigoma

Masaile Mussa – Manyara
Carolin Mpapula – Mara
Dk. Jerry Mareko – Mtwara
Christopher Kadio – Mwanza
Eric Chitindi – Njombe
Riziki Salas – Ruvuma

Makatibu katika Wizara
Andrew Masawe – Ofisi ya Waziri Mkuu
Lisante Gabriel – Wizara Uvuvi na Mifugo
Dk. Jimmy James – Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi
Edwin Muhede – Wizara Viwanda Biashara na Uwekezaji

Wakuu wa Wilaya
Jerry Murro- Arumelu
Patrobas Katambi – Dodoma
Jokate Mwegero – Kisarawe

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!