Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtuhumiwa wa kesi ya Bilionea Msuya alivyohasiwa gerezani
Habari Mchanganyiko

Mtuhumiwa wa kesi ya Bilionea Msuya alivyohasiwa gerezani

Spread the love

SHWAIBU Jumanne, maarufu kwa jina la Mredii, amenusurika kifo, lakini amepata ulemavu wa maisha. Amehasiwa na hivyo hana uwezo tena wa kupata mtoto wala kufanya tendo la ndoa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Aidha, Mredii ameishi gerezani kwa miaka mitano mfululizo, bila kuwa na kosa; na sasa ametoka akiwa hana mtaji na hana nyezo za kufanyia kazi.

Mredii, alikuwa mmoja wa washitakiwa sita waliotuhumiwa kwa mauaji ya mfanyabiashara maarufu wa Mirerani, mkoani Manyara Erasto Msuya.

Kabla ya kukutwa na dhahama hiyo, alikuwa akijishughulisha na kazi ya uchimbaji madini. Washtakiwa wenzake watano wamehukumiwa na Mahakama Kuu, kunyongwa hadi kufa.

Mbela ya Jaji Maghimbi, Mredii alinukuliwa akisema, “niliteswa na polisi hadi kupewa ulemavu, ikiwamo kuhasiwa.”

Anasema, “kipigo nilichokipata mikononi mwa polisi, kimemsababishia kilema na maumivu makubwa. Kutokana na kuhasiwa, niliamua kumpa talaka mmoja ya wake zangu, aitwaye Zuhura Hassan kwa kuwa sikuwa na uwezo tena kama mwanamume.”

Anasema, aliamua kubakiza mkewe mmoja anayeitwa Adile Juma.

Mredii anasema, hakupata matibabu mazuri kutokana na kipigo hicho na kwamba kwa vile sasa yuko huru, moja ya vipaumbele vyake, ni kupata matibabu sahihi ya afya yake.

Akiongozwa na wakili wake Majura Magafu kutoa utetezi wake, Mredii alidai mbali na kuhasiwa, polisi walimvunja mara mbili mguu wa kushoto na mara moja mguu wa kulia.

Alisema wakati fulani walimfunga kamba na kumning’iniza kama mbuzi aliyebanikwa.

“Kwa hayo mateso niliyopata hapo kituoni nimekuwa mlemavu. Niliwekwa staili ya mbuzi anayechomwa nikiwa sina nguo,” alieleza.

Anasema, mtu unapokuwa gerezani unakuchukuliwa kama mhalifu na unapokuwa kwenye lile karandinga watu wanaona wewe ni mhalifu na wengine wanakuita mwizi bila kujua ni kosa gani limekupeleka gerezani.

Waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa, ni Sharifu Mohamed, aliyekuwa mshtakiwa wa kwanza, Musa Mangu (wa tatu), Karim Kuhundwa (wa tano), Sadik Mohamed (wa sita) na Ally Mussa (wa saba), ilitolewa Julai 23 na Jaji Salma Maghimbi.

Bilionea Msuya, aliuawa kwa kupigwa risasi, tarehe 7 Agosti 2013, maeneo ya Mijohoroni wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro.

Akiongozwa na wakili wake Majura Magafu kutoa utetezi wake, tare 15 Mei mwaka huu, Mredil alitoa madai mazito mahakamani, akisema kuwa aliteswa na polisi hadi kupewa ulemavu ikiwamo kuhasiwa.

Kutokana na kuhasiwa huko, Mredil alisema, aliamua kuchukua uamuzi wa kumpa talaka moja mkewe aliyemtaja kuwa ni Zuhura Hassan kwa vile alikuwa hana uwezo tena kama mwanamme.

Alisema, mbali na kuhasiwa, lakini polisi walimvunja mara mbili mguu wa kushoto na mara moja mguu wa kulia.

Alisema, siku ya mauaji, yeye hakuwepo Arusha wala Kilimanjaro, bali alikuwa shambani kwake huko Babati akivuna mazao yake. Alisema alikuwa huko kuanzia tarehe 13 Julai hadi tarehe 7 Agosti 2013.

Shwaibu alidai alikamatwa na polisi baada ya kuitwa na mkuu wa kituo cha cha polisi (OCS) Mirerani, Ally Mkalipa, tarehe 17Agosti 2013, saa 2 usiku, na siku iliyofuata alimkabidhi kwa polisi wa Moshi.

Kutoka Polisi Mirerani, polisi walimfunga pingu na kumfunga kitambaa machoni na kupakizwa katika gari aina ya Toyota Landcruicer Hardtop na kulazwa kifudifudi hadi kituo cha polisi cha KIA.

Alidai walipofika hapo, hakuingizwa kituoni bali gari liliegeshwa nje na polisi mmoja alipotaka kumshusha, polisi mwingine alimtaka asimteremshe kwa kuwa kuna mtuhumiwa mwenzake.

Alisema kutoka kituoni hapo, polisi walimfunga pingu mikononi na kumuingiza kwenye gari na kumlaza kifudifudi na gari lilielekea hadi kituo kikuu cha polisi jijini Arusha.

Mshitakiwa huyo alidai walipofika kituoni, polisi walimfungua pingu na kumuingiza katika chumba kimoja kikubwa na walimtaka kueleza kila kitu kuhusu mauaji ya Msuya.

Kwa mujibu wa Mredil, aliwambia polisi hafahamu kitu na kwamba hakuwepo Arusha wala Kilimanjaro na hapo ndipo walipompeleka kituo cha Kisongo maarufu kwa jina la Guantaramo.

“Waliniambia hatutaki kitu kingine zaidi ya saini yako. Kwa hayo mateso niliyoyapata hapo kituoni, nimekuwa mlemavu. Niliwekwa staili ya mbuzi anayechomwa nikiwa sina nguo,” alidai.

Mredil alidaihakuwa anamfahamu mfanyabiashara Joseph Mwakipesile, maarufu kama Chussa kama maelezo ya kukiri kosa ya mshitakiwa wa kwanza, Sharifu Mohammed yaliyosomwa kortini.

“Sikuwa namfahamu kabisa Chussa zaidi ya kuona baishara zake zikiwa zimeandikwa Chussa Mining. Kwanza yeye kumuona mitaani ni vigumu kwa vile anatembea na walinzi wenye miili,” alidai.

Pia alikanusha maelezo ya onyo ya mshitakiwa wa tatu, Juma Mangu na wa saba Ally Mjeshi yaliyosomwa mahakamani yakimtaja yeye na wengine kuwa washiriki katika tukio hilo.

Mbali na maelezo hayo, mshitakiwa huyo alikanusha maelezo yaliyomo katika ungamo ya mshitakiwa wa tano, Karim Kihundwa yakidai siku ya mauaji alikuwepo eneo la tukio.

Alipoulizwa na wakili wake, Magafu kuwa anaiomba nini mahakama, ndipo shahidi huyo alipoiomba imuachie huru kwa vile hakuhusika na mauaji hayo na kesi hiyo imemtia ulemavu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

error: Content is protected !!