Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Imevuja; CAG ‘aliilewesha’ kamati iliyomuhoji
Habari za SiasaTangulizi

Imevuja; CAG ‘aliilewesha’ kamati iliyomuhoji

Prof. Mussa Assad, aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali
Spread the love

TAARIFA kutoka ndani ya kamati iliyomuhoji Prof. Mussa Assad, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) jana Jumatatu, ‘ilibaki mdomo wazi’. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Maadili amesema kuwa, Prof. Assad ni mtu makini ‘mno’ na kwamba alikuwa na majibu yaliyonyooka kwa kila swali jambo lililotosheleza wajumbe.

“Huyu anajua alichokifanya na ndio maana aliweza kujibu vizuri kila swali aliloulizwa jambo lililomtosheleza kila mmoja wetu, kila mmoja wetu alikuwa kiu yake,” ameeleza na kuongeza;

“Hatukutarajia kama atakua muungwana kwa kiwango alichoonesha. Hakuwa na hasira hata kidogo na alibaini maswali ya mtego ambayo aliyajibu vizuri.”

Pamoja na chanzo hicho kueleza kwa uchache mazingira ya kikao hicho, hakua tayari kueleza mjadala wenyewe na mwisho wake.

“Naweza kukwambia nini kimejiri lakini sitofanya hivyo kwa kuwa taarifa inapaswa kutoka kwa Spika baada ya kukabidhi ripoti hii,” kimeeleza chanzo hicho.

Yaliyoelezwa na chanzo hiki yanapata nguvu kutokana na kauli ya makamu mwenyekiti wa kamati hiyo Dk. Christine Ishengoma.

“Shahidi wetu ametoa ushahidi mkubwa sana. Tumemuhoji na amerujibu maswali yetu kama alivyoulizwa,” alisema Dk. Ishengoma baada ya kumaliza mahojiano na CAG.

Hata hivyo chanzo hichi kimeeleza kuwa, katika mahojiano hayo kilichotawala ni uungwana kwa pande zote mbili yaani upande wa shahidi na kamati.

“Tofauti kabisa na taarifa za awali katika vyombo vya habari na mitandaoni, hakuna jambo lililoinekana kuwa gumu kwenye kikao hicho.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!