Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko IGP Sirro aagiza aliyetishia kwa bastola, akamatwe
Habari Mchanganyiko

IGP Sirro aagiza aliyetishia kwa bastola, akamatwe

IGP Simon Sirro
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro amesema kijana aliyefahamika kwa jina moja la Shaban, atakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani, kwa kosa la kumtishia mwenzake na bastola. Anaripoti Martin Kamote … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 1 Novemba 2019 jijini Dar es Salaam, IGP Sirro amesema mtu anayekiuka masharti ya kumiliki silaha, hunyang’anywa silaha na kufikishwa mahakamani .

“Kimsingi mtu unapopewa silaha ufuate hayo masharti, usipofuata masharti  la kwanza, tutakunyang’anya silaha,  la pili tutakupeleka mahakamani, la tatu tutamuomba Mungu atusaidie tukufunge ili ukirudi nyumbani kwako uwe na adabu ya kutumia silaha,” amesema IGP Sirro.

IGP Sirro amemtaka Shaban kujisalimisha katika kituo cha polisi, sambamba na kusalimisha silaha yake.

Amesema,  Shaban amekiuka masharti ya kumiliki silaha, kufuatia hatua yake ya kumtishia mwenzie, aliyekuwa anajibizana nae.

“Sisi silaha tuliwapa kwa masharti maalumu,  hatukuwapa silaha kwa ajili ya kutishia Watanzania, tukibaini umetishia watanzania kama alivyofanya yule  kijana, hatujui ugomvi ulikuwa ni nini. Lakini je,  kama ni kweli yale yaliyokuwa yanaelezwa,  alikuwa na sababu za kutoa silaha kumtishia mwenzake?” amehoji IGP Sirro.

Hivi karibuni ilisambaa video katika mitandao ya kijamii, inayomuonesha Shaban akitishia kumdhuru na bastola, mwanaume ambaye jina lake halijafahamika.

Kitisho hicho cha Shaban kilifuata kutokana na majibizano yaliyozuka baina yake na huyo mwenzie.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!