Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko IGP awasimamisha kazi askari waliohusika mauji Kilombero kupisha uchunguzi
Habari Mchanganyiko

IGP awasimamisha kazi askari waliohusika mauji Kilombero kupisha uchunguzi

IGP, Camilius Wambura
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania, IGP Camillus Wambura, amewasimamisha kazi askari wote waliohusika na tukio la mauji ya raia wawili yaliyotokea tarehe 23 Oktoba, 2022 katika Kijiji cha Ikwambi Kata ya Mofu wilayani Kilombero mkoani Morogoro, ili kupisha uchunguzi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mauji hayo yalitokea kufuatia vurugu za wananchi jamii ya wafugaji na wakulima ambao walikuwa wanalalamikia mifugo kuingizwa kwenye mashamba yao na wenzao wawili kushambuliwa.

Kwa mujibu wa taarifa ya IGP Wambura aliyoitoa leo Jumatatu tarehe 24 Oktoba, 2022, amesema ameunda timu ya uchunguzi itakayoongozwa na Mkurugenzi wa Mashitaka  pamoja na taasisi zingine za Serikali ili kufanya uchunguzi huru.

Amesema katika taarifa yake hiyo kuwa lengo la uchunguzi huo ni kupata majibu ya chanzo cha tukio hilo na kubaini uwiano wa matumizi ya nguvu iliyotumiwa na Jeshi la Polisi katika kudhibiti vurugu na endapo zilienda sambamba na vurugu zenyewe.

“Nimeelekeza kuwa askari wote waliohusika kwenye tukio hilo wakae kando kupisha uchunguzi ili timu hii huru iwe na nafasi nzuri ya kuweza kutimiza wajibu wake na kuweza kuja na majibu na matokeo sahihi ya uchunguzi huo kwa jamii ili Watanzania waweze kufahamu ukweli wa tukio hilo.

“Endapo  kutabainika mapungufu, madhaifu au chochote kile amabcho kinaonesha uzembe kwa upande wa yeyote yule, basi hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi yake,” amesema Wambura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!