BENKI ya Exim tawi la Mwanza imekabidhi msaada wa majaketi yenye viakisi mwanga (Reflector Jackets) kwa madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda wa mkoani humo ikiwa ni sehemu ya jitihada ya benki hiyo katika kukabiliana na ajali za barabarani zinazotokea mkoani humo
hususani nyakati za usiku. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Hafla ya makabidhiano ya majaketi hayo ilifanyika kwenye tawi la benki hiyo mkoani humo na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo maofisa wa benki hiyo wakiongozwa na Meneja wa Benki hiyo tawi la Mwanza, Edwin Polle, Meneja Mahusiano wa benki hiyo mkoa wa Mwanza, Sarah Tito, wawakilishi kutoka jeshi la Polisi, kikosi cha Usalama Barabarani wakiongozwa na Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa Mwanza, ASP. Sunday Ibrahim pamoja na wawakilishi wa madereva wa pikipiki mkoa huo.
Leave a comment