Kivumbi cha michuano ya Euro kitaanza kutimua vumbi kesho, ambapo kutapigwa mchezo mmoja wa kundi A, kati ya Uturuki dhidi ya Italy. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Michuano hiyo itashikilisha timu 24, ambapo ilitakiwa kufanyika mwaka jana na kuahirishwa mara baada ya mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya Corona.
Ratiba ya michuano hiyo pia, itaendelea jumamosi ambapo itapigwa michezo mitatu, Wales wataikabili Uswis, Denmark dhidi Finland na Ubeligiji watamenyana na Urusi.
Bingwa mtetezi timu ya Taifa ya Ureno ambayo ipo kundi F, itashuka dimbani siku ya Jumanne dhidi ya Hungary.
Leave a comment