Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Michezo Dube kupelekwa Afrika Kusini kwa matibabu
Michezo

Dube kupelekwa Afrika Kusini kwa matibabu

Prince Dube
Spread the love

MSHAMBULIAJI wa Azam FC na timu ya Taifa ya Zimbabwe, Price Dube ataondoka nchini Jumapili ya tarehe 29 Novemba, 2020, kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu mara baada ya kuumia kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Yanga uliochezwa jana. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo ambao ulimalizika kwa Azam FC kupoteza kwa bao 1-0, kwenye dakika 48 likifungwa na Deus Kaseke na kuifanya Yanga kuibuka na pointi tatu na kukaa juu kwenye msimamo wa Ligi.

Dube aliumia dakika ya 15 ya mchezo kwa kuvunjika mfupa wa mbele wa mkono wakati alipoanguka vibaya wakati akiwania mpira wa juu na beki wa kati ya Yanga, Bakari Mwamnyeto na kutolewa nje na nafasi yake kuchukuliwa na Richard Djodi.

Taarifa kutoka ndani ya Azam FC imeeleza kuwa mara baada ya kuumia Dube alipatiwa huduma ya kwanza na baadae kupelekwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Dube ataondoka na Shirika la ndege la Kenya na atapatiwa matibabu kwenye hospitali ya Vincent Pallotti iliyopo kwenye mji wa Cape Town, Afrika Kusini chini ya daktari bingwa wa mifupa Robert Nicolas.

Mshambuliaji huyo alijiunga na timu hiyo wakati wa dirisha kubwa la usajili akitokea klabu ya Highlanders FC inayoshiriki Ligi Kuu nchini Zimbabwe.

Mpaka sasa Dube ameshapachika jumla ya mabao sita na kuwa kinara wa mabao ndani ya klabu yake, huku akiwa nyuma kwa bao moja na kinara wa mabao wa Ligi Kuu, John Bocco mwenye mabao saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!