Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mollel: Wananchi hawataki katiba mpya, wanataka maendeleo
Habari za Siasa

Dk. Mollel: Wananchi hawataki katiba mpya, wanataka maendeleo

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto nchini Tanzania, Dk. Godwin Mollel
Spread the love

 

NAIBU Waziri wa Afya, Dk. Godwin Mollel, amedai kwamba wananchi hawataki katiba mpya, bali wanataka maendeleo na huduma bora za kijamii. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara … (endelea).

Dk. Mollel ametoa kauli hiyo leo Jumatatu, tarehe 26 Julai 2021, katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini, mkoani Mtwara.

Naibu waziri huyo wa afya, amedai kuwa, wananchi wanaunga mkono msimamo wa Serikali wa kuweka kando mchakato wa upatikanaji katiba mpya, ili kuimarisha maendeleo ya nchi.

“Vijana wa Tanzania wako pamoja na nyie, nimezungumza katika ziara yangu jimboni kwangu na katika mikoa mitano, hakuna anayezungumzia katiba mpya, wote wanataka dawa, maji, huduma bora za afya na kupunguza vifo vya kina mama na watoto,” amesema Dk. Mollel.

Dk. Mollel amesema kuwa, badala ya Serikali kutumia fedha katika kuendesha Bunge la Katiba, ipeleke fedha hizo katika miradi ya maendeleo.

“Badala ya sisi kukaa bungeni kutumia fedha kutunga katiba mpya, fedha hizo mmeamua kutupa Sh. 6.5 bilioni, tuwanunulie watu wa Mtwara vifaa tiba na hospitali yao ianze,” amesema Dk. Mollel na kuongeza:

“ Badala ya sisi kutumia pesa kwenda kukaa kujadili katiba, mmeamua kutoa Sh. 157 bilioni zijenge bandari Mtwara, ambayo haitagusa watu wa korosho peke yake, itaongeza ajira kwa vijana.”

Kauli hiyo ya Dk. Mollel imekuja huku kukiwa na vuguvugu la madai ya katiba mpya, yaliyoibuliwa na baadhi ya makundi hasa ya vyama vya siasa na asasi za kiraia.

1 Comment

  • Katiba ya Tanzania ya sasa siyo Katiba ya wananchi… ni Katiba iliyotokana na sheria za kikoloni na mfumo wa chama kimoja. Maendeleo hayaji bila Katiba nzuri. Ndiyo maana hatuendelei kulinganana rasilimali zilizoo wala kujua mikataba ya madini ni ya miaka mingapi.
    Wachina waliambiwa watarejeshewa Hong Kong baada ya miaka 90. Madini vipi?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!