KATIBU Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo amemuagiza Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila kuhakikisha mabasi ya mwendokasi yanarejeshwa katika njia ya kuelekea Mbagala ili kunusuru wananchi wa ukanda huo na adha ya usafiri. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Tarehe 27 Juni 2023 safari za mabasi hayo kati ya Gerezani hadi Mbagala rangi tatu ambayo ililenga kurahisisha huduma ya usafiri kwa watu wanaotaka kutembelea maonyesho ya sabasaba.
Hata hivyo, akizungumza katika mkutano wa CCM uliofanyika katika viwanja vya Kawe jijini Dar es Salaam, Chongolo amesema si nia ya serikali kutoa huduma kwa kipindi kifupi kifupi pekee kwa wananchi.
Ameeleza kushangazwa na Wakala wa Mabasi yaendayo Haraka (DART) maarufu kwa jina la Mwendokasi kusitisha huduma hiyo baada ya maonesho ya sabasaba kumalizika.
“Wekeni utaratibu mabasi yaendelee kutoa huduma Mbagala ili wanachi waondokane na utaratibu wa kupitia madirisha, watu wanufaike na maendeleo ya huduma za miundombinu.
“Kama mabasi ni machache, wekeni mpango haraka wa kuongeza mabasi kwa sababu Serikali imetumia mabilioni ya fedha kujenga barabara hizo,” amesema.
Amesema kazi CCM sio kusema watafanya bali pia wanataka kuona mambo yakienda kwa haraka kwa ufanisi unaotakikana.
Leave a comment