Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chanzo kifo cha Mbunge CCM aliyefariki ghafla hotelini, chaanikwa
Habari za Siasa

Chanzo kifo cha Mbunge CCM aliyefariki ghafla hotelini, chaanikwa

Spread the love

HOSPITALI ya Rufaa ya Sokoine mkoani Lindi, imesema chanzo cha kifo cha Rashid Akbar, aliyekuwa Mbunge wa Newala Vijijini, kilichotokea ghafla jana tarehe 15 Januari 2020, ni ugonjwa wa moyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Chanzo hicho kimetangazwa na Dk. Nicholas Mmuni, Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, baada ya mwili wa Akbar kufanyiwa uchunguzi kuhusu chanzo cha kifo chake.

Dk. Mmuni ameeleza kuwa, kabla ya umauti kumfika, Akbar alisumbuliwa kwa muda mrefu na maradhi ya moyo, na kupelekea kuwekewa mashine maalumu mwilini mwake, iliyokuwa inasaidia moyo wake kufanya kazi (Pacemaker).

“Baada ya mwili wake kupokelewa hospitalini hapa uchunguzi ulifanyika na kubainisha kwamba amefariki dunia kutokana na maradhi ya moyo yaliyokuwa yanamsumbua muda mrefu. 

Ambayo yalipelekea kuwekewa mashine iliyokuwa inamsaidia moyo kufanya kazi vizuri, (pacemaker) ambacho alikuwa akitembea nacho ndani ya mwili wake siku zote, ameeleza Dk. Mmuni. 

 Marehemu Akbar alifariki dunia jana akiwa hotelini kwake Mingoyo iliyoko maeneo ya Mnazi Mmoja mkoani humo.

Mwili wake unatarajiwa kuzikwa leo tarehe 16 Januari 2020 majira ya saa saba mchana.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!