Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yaijibu CCM mashambulizi dhidi ya Rais Samia
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yaijibu CCM mashambulizi dhidi ya Rais Samia

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema maridhiano yanayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan, hayatazuia kuikosoa Serikali yake katika mikutano ya hadhara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita…(endelea).

Msimamo huo umetolewa leo tarehe 31 Julai 2023 na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu, katika mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika mkoani Geita.

Baada ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuituhumu Chadema kwamba wanatumia mikutano ya hadhara kutoa kauli za kejeli dhidi ya Rais Samia, licha ya mema aliyowafanyia ikiwemo kuwapa ruzuku na kuwatoa vifungoni wafuasi wake.

“Ukitufunga bure tutakusema, ukituachia tutakusema, ukiiba tutakusema, ukigawa nchi yetu tutakusema na tutakusema mchana kweupe. Sisi hatuhongeki kama mlifikiri mnatuachia kama hongo hiyo haipo,” amesema Lissu na kuongeza:

“Mlichofanya hamjatupa chochote ambacho sheria za Tanzania zinasema sio za kwetu, sheria inasema  kufanya mikutano ni halali hivyo hamkutupa fadhila mliondoa haram mliyoweka wenyewe. Kazi ya mikutano ni kueleza wananchio ubovu ulioko madarakani ndiyo kazi yetu, kutakuwa na haja gani kufanya mikutano kwenda kumsifu mama hata anapofanya mambo ya hovyo.”

Jana Jumapili, akizungumza katika mkutano wa hadhara mkoani Tabora, Kinana aliitaka Chadema isitumie vibaya fursa ya kufanya mikutano ya hadhara kutukatan, kudharau na kukejeli Serikali ya Rais Samia.

“Tumekaa nao tangu Mei 2022 mpaka kikao cha mwisho Juni 2023, hakuna ajenda hata moja imetoka kwa CCM kwenda mezani, zote zimetoka kwao na nyingi tumezifanyia kazi, walikuwa wanachama wao wana kesi nyingi zimetazamwa na nyingine zimefutwa, jamani yote haya hayafai? Hayastahili kushukuriwa? Hayastahili Rais kuheshimiwa?” Kinana alihoji.

Mwanasiasa huyo alisema “Tumefungua mikutano kuja kusemwa, kusakamwa na kudhalilishwa? tumetoa ruzuku waliyoomba kusafiria kupata fursa ya kwenda kutusema na kututukana? Hatusemi tunafanya hisani lakini tumekuwa waungwana.”

Kinana aliitaka Chadema kuwa waungwana kwa kufanya siasa zenye hoja badala ya kujenga hoja kwa dharau.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!