Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema wamtega Msajili wa vyama
Habari za SiasaTangulizi

Chadema wamtega Msajili wa vyama

Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi
Spread the love

 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema hakitashiriki vikao vya majadiliano ya wadau wa vyama vya siasa, vilivyoitishwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, hadi mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, atakapoachwa huru bila masharti yoyote. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Sharti hilo limetajwa leo Jumatatu, tarehe 11 Oktoba 2021 na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, Benson Kigaila, akitoa maazimio ya kikao cha kamati kuu ya chama hicho, kilichofanyika jana Jumapili, kwa njia za kidigitali.

“Sisi kama Chadema hatuwezi kwenda kwenye vikao vya msajili, mpaka mwenyekiti wetu aachiwe bila masharti yoyote. Sababu Watanzania, Serikali na dunia inajua kwamba Mbowe sio gaidi amebambikiziwa kesi kwa lengo la kumtesa,” amesema Kigaila.

Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu Chadema Bara

Kigaila amesema, Chadema hakiwezi kushiriki kikao hicho wakati mwenyekiti wake yuko ndani.

“Hatuwezi kwenda kwenye kikao kujadiliana chochote wakati kiongozi wetu yuko ndani, tunataka Serikali ifute mashtaka ya kubumba waliyomtengenezea mwenyekiti wetu atoke, aachwe huru ili kama kuna vikao vya kwenda twende naye,” amesema Kigaila.

Msimamo huo umetolewa katika kipindi ambacho Jaji Mutungi ameitisha kikao cha wadau wa vyama vya siasa, ikiwemo Inspekta wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro, ili kutafuta suluhu ya changamoto zinazokabili tasnia hiyo.

Kikao cha wadau wa vyama vya siasa nchini, kinatarajiwa kufanyika jijini Dodoma, tarehe 21 Oktoba 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!