Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Carlinhos avunja mkataba Yanga, asepa zake
Michezo

Carlinhos avunja mkataba Yanga, asepa zake

Carlos Stenio Fernandes 'Carlinhos'
Spread the love

 

UONGOZI wa klabu ya Yanga umethibitisha kuvunja mkataba na kiungo wake Raia wa Angola, Carlos Stenio Fernandes ‘Carlinhos’ mara baada ya makubaliano ya pande zote mbili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Carlinhos ambaye alijiunga Yanga kwa mkataba wa miaka miwili kwenye msimu wa 2020/21 akitokea nchini Angola amevunja mkataba huo kutokana na sababu za kifamilia.

Mchezaji huyo aliondoka nchini jana usiku nakurejea kwao Angola mara baada ya kuitumikia Yanga katika kipindi cha msimu mmoja tu.

Taarifa kutoka kwenye uongozi wa klabu ya Yanga ilieleza kuwa makubaliano ya kuvunja mkataba ulifikiwa na pande zote mbili kwa ajili ya manufaa ya klabu mara baada ya mchezaji huyo kuwasilisha ombi la kuondoka.

Katika kipindi cha msimu mmoja aliokaa Yanga Carlinhos hakuitumikia kwa muda mrefu timu hiyo kutokana na kuandamwa na majeruhi ya mara kwa mara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!