Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari CAG abaini kasoro michezo ya kubahatisha
Habari

CAG abaini kasoro michezo ya kubahatisha

Spread the love

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Charles Kichere amebaini ufanisi duni kwenye mchakato wa utoaji leseni kwa waendeshaji wa michezo ya kubahatisha hali inayoweza kuwa hatari kwa wateja wao. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kichere amebaini hayo kupitia ripoti zake za mwaka 2020/21 alizozifanya akisema, ukaguzi alioufanya kwa mashirika ya udhibiti yenye mamlaka ya kutoa leseni ulibaini mapungufu kadhaa yakiwamo Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT) kutoa leseni kwa waendeshaji 60 wa michezo hiyo bila ya amana ya kutosha.

Anasema, amana ni kama dhamana ya usalama na ulinzi kwa ajili ya kuwalinda wateja wa michezo hiyo.

Kichere anasema, amana hiyo inaweza kutumika inapotokea waliopewa leseni za uendeshaji wa michezo hiyo wameshindwa kulipa madeni ya wateja wao kama inavyotakiwa na Kifungu cha 18A cha Sheria ya Michezo ya Kubahatisha [kama ilivyorekebishwa mwaka 2019].

“Kwa kutowasilisha dhamana, bodi haiwezi kuwalinda wadau wa michezo ya kubahatisha iwapo waendeshaji wa michezo hiyo wataingia kwenye madeni na wateja wao,” anasema Kichere kwenye ripoti ya Mashirika ya Umma na kuongeza:

“Ninapendekeza Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania ihakikishe waendeshaji wa michezo ya kubahatisha wana kiwango cha dhamana cha kutosha ili kulinda wateja iwapo mwenye leseni atashindwa kulipa madeni ya michezo ya kubahatisha.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!