Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko BoT yakunjua makucha, yafunga benki tano
Habari Mchanganyiko

BoT yakunjua makucha, yafunga benki tano

Benki Kuu ya Tanzania
Spread the love

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imezifunga na kuziweka chini ya ufilisi benki tano nchini kutokana na kuwa na upungufu wa mtaji kinyume na matakwa ya sheria. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Sheria iliyovunjwa na ile ya benki na taasisi za fedha ya mwaka 2006 na kanuni zake.

Uamuzi huo umetolewa leo na BoT na kwamba imefanya hivyo kwa mamlaka iliyopewa chini ya kifungu cha 56(1)(g), 56(2) (a), (b) na (d), 58(2)(i), 11(3)(c) na (j), 61(1) na 41(a) cha sheria ya benki na taasisi za fedha ya mwaka 2006.

Imezitaja benki hizo kuwa ni Covenant Bank For Women (T) Limited, Efatha Bank Limited, Njombe Community Bank Limited, Kagera Farmers’ Cooperative Bank Limited, na Meru Community Bank Limited.

“Kwa mamlaka iliyopewa chini ya kifungu Na. 41(a) cha sheria ya benki na taasisi za fedha ya mwaka 2006; Benki Kuu ya Tanzania imeiteua Bodi ya Bima ya Amana (The Deposit Insurance Board) kuwa mfilisi kuanzia leo tarehe 04 Januari 2018.

“Uamuzi huu umechukuliwa baada ya Benki Kuu ya Tanzania kujiridhisha kuwa benki hizi zina upungufu mkubwa wa mtaji kinyume na matakwa ya sheria.

Taarifa ya BoT imeeleza kuwa upungufu huo wa mtaji unahatarisha usalama wa sekta ya fedha na kwamba kuendelea kutoa huduma za kibenki kwa benki hizo kunahatarisha usalama wa amana za wateja wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!