MARA baada ya kuahirisha mchezo dhidi ya Yanga bodi ya Ligi Kuu imeahirisha tena mchezo wa Simba dhidi ya Coastal union kutoka Tanga kutoka na Simba kuwa safarili kuelekea nchini Afrika kusini kwenye mchezo dhidi ya Kaizer Chiief utakaopigwa Tarehe 15 Mei 2021. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)
Mchezo huo ulipangwa kuchezwa Tarehe 11 Mei 2021, kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
Simba itaondoka kesho jumanne majira ya saa 9 usiku kuelekea Afrika kusini wakipitia Kenya kwenye mchezo wa Robo Fainali ya klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Kaizer Chiefs.
Barua ya Bodi ya ligi kwenda kwa katibu wa klabu ya Coastal union imeeleza kuwa mchezo huo utapangiwa siku nyingine.
Leave a comment