Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Biashara United yaanza mwaka kwa Tuzo
Michezo

Biashara United yaanza mwaka kwa Tuzo

Spread the love

 

MSHAMBULIAJI wa Biashara United ya Mara, Deogratius Mafie amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa mwezi Januari wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) msimu wa 2020/21, huku Francis Baraza pia wa Biashara United akichaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mafie na Baraza walitwaa tuzo hizo, baada ya kuwashinda wenzao walioingia nao fainali kwa mwezi Januari katika uchambuzi uliofanywa wiki hii na Kamati ya Tuzo za VPL, kutokana na mapendekezo ya makocha waliopo vituo mbalimbali ambavyo ligi hiyo inachezwa.

Mafie aliwashinda kiungo wa Ruvu Shooting, Mohammed Issa na mshambuliaji wa Mwadui FC, Wallace Kiango, huku Baraza akiwashinda Charles Mkwassa wa Ruvu Shooting na Abdallah Mohammed wa JKT Tanzania.

Wachezaji wengine ambao tayari wameshatwaa tuzo hiyo ya mwezi kwa msimu huu na miezi yao katika mabano ni Prince Dube wa Azam (Septemba), Mukoko Tonombe wa Yanga (Oktoba), John Bocco wa Simba (Novemba) na Saidi Ntibazonkiza wa Yanga (Desemba).

Makocha waliotwaa tuzo hiyo ni Aristica Cioaba aliyekuwa Azam (Septemba), Cedric Kaze wa Yanga (Oktoba), Charles Mkwassa wa Ruvu Shooting (Novemba) na Cedrick Kaze  wa Yanga (Desemba).

TFF na Bodi ya Ligi zimekuwa na utaratibu wa kutoa Tuzo ya Mchezaji Bora na Kocha Bora wa VPL kila mwezi, ambapo pia mwisho wa msimu kunakuwa na tuzo za wachezaji mbalimbali waliofanya vizuri kwa msimu mzima, ikiwemo Tuzo ya Mchezaji Bora wa msimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!