Wednesday , 6 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Basi la Magereza lagonga treni yenye abiria 650 Dar
Habari MchanganyikoTangulizi

Basi la Magereza lagonga treni yenye abiria 650 Dar

Spread the love

Basi  Jeshi la Magereza lenye namba MT 0040 limegonga treni ya abiria namba YD16 yenye injini namba 9015 iliyokuwa ikitokea mikoa ya Bara (Morogoro, Dodoma, Tabora na Kigoma) katika eneo la Ukonga jjini Dar es Salaam, muda wa saa 11:25 leo Ijumaa  jioni. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Basi hilo la Magereza lililokuwa limebeba watu 15 liliigonga na treni namba YD16 yenye injini namba 9015 iliyobeba abiria 650 wakati basi hilo likivuka reli eneo la Kilomita 13 (Ukonga Magereza).

Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano kutoka Shirika la Reli Tanzania, Jamila Mbarou imesema ajali hiyi imesababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi 10 ambao kati yak wanawake watano na wanaume watano.

Amesema majeruhi wamewahishwa katika Hospitali ya Amana kwa ajili ya matibabu.

“Shirika linaendelea kuwasihi madereva wa vyombo vya moto kuwa makini wanapokatiza reli kufuata Sheria na alama za usalama wa reli zilizowekwa ili kuepusha ajali.

“Shirika linatoa pole kwa ndugu wa marehemu na Mwenyezi Mungu awape nafuu majeruhi ili waweze kuendelea na shughuli za kujenga Taifa, taarifa zaidi zitaendelea kutolewa,” amesema.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Shura ya Maimamu kukata rufaa kupinga Sheikh kufungwa miaka 7

Spread the loveSHURA ya Maimamu Tanzania, inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu...

BiasharaTangulizi

Bei ya Dizeli, Petroli yashuka

Spread the loveBEI ya mafuta kwa mwezi Disemba, imeshuka kutokana na kupungua...

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

error: Content is protected !!