Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Baraza Kuu Chadema: Ni Lissu, Nyalandu
Habari za Siasa

Baraza Kuu Chadema: Ni Lissu, Nyalandu

Wajumbe wa Baraza Kuu la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wakisubiri kuanza kwa kikao hicho
Spread the love

BARAZA Kuu la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinafanyika leo Jumatatu tarehe 3 Agosti 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kikao hicho, kinafanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam kikiwa na kazi ya kupendekeza majina ya wagombea urais wa Tanzania, mgombea mwenza na wa Zanzibar.

Pia, baraza hilo litapendekeza, Ilani ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Tayari wajumbe wameanza kuingia ukumbini kuhudhuria mkutano huo huku majina ya Tundu Lissu na Lazaro Nyalandu yakisikika zaidi kati ya wagombea saba wanaowania kupitishwa na chama hicho kugombea urais wa Tanzania.

MwanaHalisi Online lipo ukumbini kufuatilia kinachoendelea na litakuletea taarifa na habari mbalimbali.

Meza kuu ya Baraza Kuu la Chadema ikiwa wazi kabla ya viongozi wake kuingia ukumbini

Baadhi ya wajumbe waliozungumza na MwanaHALISI Online wakiomba hifadhi ya majina yao wamesema, kuna mchuano mkali kati ya Lissu ambaye ni makamu mwenyekiti wa Chadema-Bara na Nyalandu, mwenyekiti wa chama hicho kanda ya kati.

“Aise, sijajua nani ataibuka kati ya Lissu au Nyalandu. Ila dalili ukiona kama Lissu anapenya lakini Nyalandu hayuko nyuma sana. Amejipanga vizuri na lolote linaweza kutokea,” amesema mjumbe huyo wa baraza kuu kutoka kanda ya Serengeti

Mjumbe wa kanda ya Pwani amesema,”hakuna ubishi katika hili, Lissu ndiye tunayemta. Anayeweza mikiki mikiki.”

Hadi saa 6:45 mchana, kikao hakijaanza.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV, kwa habari, taarifa mbalimbali

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!