Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Balozi Mndolwa: Msiwachukie wapinzani
Habari za Siasa

Balozi Mndolwa: Msiwachukie wapinzani

Spread the love

 

BALOZI Fransic Mndolwa, ameshauri wanasiasa wa vyama vya upinzani wasichukiwe bali wapendwe, akisema wana msaada katika Taifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Balozi Mndolwa ametoa wito huo leo Jumatatu, tarehe 6 Desemba 2021, katika Kongamano la Kitaifa la Miaka 60 ya Uhuru, lililofanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), jijini Dar es Salaam.

Tanzania Bara inatarajia kutimiza miaka 60 ya uhuru, tarehe 9 Desemba mwaka huu, ambapo ilipata uhuru wake kutoka kwa Uingereza, tarehe 9 Desemba 1961.

“Bahati nzuri tunakwenda vizuri wala msiogoe vitu vidogo, ambavyo vinajitokeza, unasikia vyama vya upinzani vinalaumu huku na huko. Wala msiwachukie wapinzani, muwapende kwa sababu wanatusaidia kutuchangamsha tufikirie zaidi,” amesema Balozi Mndolwa.

Balozi huyo amesema, ili kulinda heshima ya Tanzania katika mahusiano ya kimataifa, inatakiwa iondoe tofauti zake.

“Ushirikiano wa kimataifa uimarishwe na utaimarika kama ndani ya nchi na sisi wenyewe tunakazana kutoa tofauti zetu na kujiimarisha. Hatuwezi kuwasaidia wengine wa nje kama humu ndani wenyewe tunavurugana,” amesema Balozi Mndolwa.

Akizungumzia miaka 60 ya uhuru wa Tanzania Bara, Balozi Mndolwa amesema Watanzania wanatakiwa kuenzi amani na utulivu, uliodumu katika kipindi hicho.

“Tunao mtihani mkubwa kuhakikisha tunayamudu maisha ya amani kwa miaka mingine 60 ijayo, miaka 60 tuliweza kukaa tulivyokaa na sasa tunaanza muhula mwingine wa miaka 60,” amesema Balozi Mndolwa na kuongeza:

“Hakuna budi kuongeza juhudi kuhakikisha tunaishi kwa amani kama tulivyoishi miaka 60 iliyopita.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!