Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bajeti 2020/21: TRA kukusanya mapato ya utalii Tanzania
Habari za Siasa

Bajeti 2020/21: TRA kukusanya mapato ya utalii Tanzania

Watalii wakiwa moja ya mbuga nchini Tanzania
Spread the love

SERIKALI  ya Tanzania imependekeza mfumo wa ukusanyaji wa mapato yanayotokana na sekta ya utalii na mazao ya misitu nchini humo kufanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa mwaka wa fedha 2020/21. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango leo Alhamisi tarehe 11 Juni 2020 Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha bajeti ya serikali ya mwaka 2020/21 ya Sh. 34.87 Trilioni.

Dk. Mpango amesema, katika kuboresha mfumo wa ukusanyaji wa maduhuli yanayotokana na sekta ya utalii na mazao ya misitu, Serikali inapendekeza ukusanyaji wa maduhuli hayo ufanywe na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na mapato hayo yaingie katika Mfuko Mkuu wa Hazina.

Amesema, utekelezaji wa hatua hii utahusisha marekebisho katika Sheria ya Mamlaka ya Mapato Tanzania, Sura 399, Sheria ya Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro, Sura 284, Hati ya Kuanzisha Mamlaka ya Hifadhi ya Wanyamapori ya mwaka 2014, na Sheria ya Hifadhi za Taifa, Sura 282 kupitia Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2020 (The Finance Bill, 2020) ili:

(i) Kuipa TRA mamlaka kisheria ya kukusanya maduhuli yanayokusanywa hivi sasa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), na Mamlaka ya Hifadhi ya Wanyamapori (TAWA);

(ii) Kuweka sharti la kisheria ili kuwezesha maduhuli yatakayokusanywa na TRA yahifadhiwe Mfuko Mkuu wa Hazina badala ya utaratibu wa sasa unaoruhusu taasisi hizi kubaki na mapato yake;

(iii) Kuweka utaratibu wa kisheria kwa taasisi hizo kutumia utaratibu wa bajeti ya Serikali na kuondoa mfumo wa kibajeti unaotumiwa na taasisi hizo kwa sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!