Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Auawa kwa tuhuma za ujambazi
Habari Mchanganyiko

Auawa kwa tuhuma za ujambazi

Spread the love

MTU mmoja anayefahamika kwa jina la Mussa Faustine (19) mkazi wa Bugarika wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza, ameuawa na wananchi wenye hasira kali kwa tuhuma za ujambazi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 28 Julai, 2018, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi amesema Faustine amefariki dunia akiwa njiani kuelekea hospitali kutokana na majeraha ya kipigo cha wananchi,  baada ya kuhojiwa na askari polisi.

Kamanda Msangi amesema kabla ya mtuhumiwa huyo umauti kumfika aliutaja mtandao sugu wa ujambazi na kiongozi wake anayefahamika kwa jina la Hamza, ambao ulipanga kutekeleza matukio mengine ya ujambazi hivi karibuni.

“Kijana huyo alitoa ushirikiano vizuri kwa askari japo alikuwa katika hali ya kujeruhiwa sana, alitoa ushirikiano na kueleza kikundi chake ambacho wanashirikiana katika kufanya na kupanga matukio ambayo walikuwa wamepanga kufanya katika siku za hivi karibuni kisha alimtaja kiongozi wake aitwaye hamza maarufu mjomba,” amesema Kamanda Msangi.

Vile vile, Kamanda Msangi amesema marehemu Faustine aliwapeleka polisi maeneo wanakoficha silaha, ambapo polisi baada ya kufanya upekuzi walikuta silaha nne zilizotengenezwa kienyeji na risasi saba.

Kamanda Msangi amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya rufaa ya Bugando kwa ajili ya uchunguzi na kwamba uchunguzi ukikamilika utakabidhiwa kwa ndugu zake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!