Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Auawa kwa tuhuma za ujambazi
Habari Mchanganyiko

Auawa kwa tuhuma za ujambazi

Spread the love

MTU mmoja anayefahamika kwa jina la Mussa Faustine (19) mkazi wa Bugarika wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza, ameuawa na wananchi wenye hasira kali kwa tuhuma za ujambazi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 28 Julai, 2018, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi amesema Faustine amefariki dunia akiwa njiani kuelekea hospitali kutokana na majeraha ya kipigo cha wananchi,  baada ya kuhojiwa na askari polisi.

Kamanda Msangi amesema kabla ya mtuhumiwa huyo umauti kumfika aliutaja mtandao sugu wa ujambazi na kiongozi wake anayefahamika kwa jina la Hamza, ambao ulipanga kutekeleza matukio mengine ya ujambazi hivi karibuni.

“Kijana huyo alitoa ushirikiano vizuri kwa askari japo alikuwa katika hali ya kujeruhiwa sana, alitoa ushirikiano na kueleza kikundi chake ambacho wanashirikiana katika kufanya na kupanga matukio ambayo walikuwa wamepanga kufanya katika siku za hivi karibuni kisha alimtaja kiongozi wake aitwaye hamza maarufu mjomba,” amesema Kamanda Msangi.

Vile vile, Kamanda Msangi amesema marehemu Faustine aliwapeleka polisi maeneo wanakoficha silaha, ambapo polisi baada ya kufanya upekuzi walikuta silaha nne zilizotengenezwa kienyeji na risasi saba.

Kamanda Msangi amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya rufaa ya Bugando kwa ajili ya uchunguzi na kwamba uchunguzi ukikamilika utakabidhiwa kwa ndugu zake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!