Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Umoja wa Mataifa kununua tani mil 3 za chakula
Habari Mchanganyiko

Umoja wa Mataifa kununua tani mil 3 za chakula

Mahindi yakiwa shambani
Spread the love

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limewatangazia neema wakulima wa mazao ya chakula nchini, ambapo imewahakikishia kwamba itanunua chakula cha ziada kitakachozalishwa zaidi ya tani milioni 3. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Hayo yamesemwa leo terehe 27 Julai, 2018 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa baada ya kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa WFP, Bw. David Beasley, jijini Dar es Salaam.

Waziri Majaliwa amesema Beasley amemhakikishia kwamba shirika lake litayanunua mazao hayo, na hivyo kupunguza tatizo la ukosefu wa masoko kwa wakulima.

“Taarifa za Wizara ya Kilimo zinaonesha kuwa mavuno ya mazao ya chakula kama mahindi, maharage na mbaazi yatafikia tani milioni 16 wakati mahitaji ya chakula kwa Watanzania kwa mwaka ni tani milioni 13, hivyo tutakuwa na ziada ya tani milioni tatu,” amesema.

Vile vile, Waziri Majaliwa amesema ujio wa Beasley hapa nchini ni fursa itakayowawezesha Watanzania kunufaika kwa kiwango kikubwa katika kilimo, uhifadhi na uuzaji wa mazao ya chakula yanayolimwa hapa nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!