Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Ruwa’ichi: Tuishi kama wapita njia
Habari Mchanganyiko

Askofu Ruwa’ichi: Tuishi kama wapita njia

Spread the love

 

ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Yuda Thadeus Ruwa’ichi, amewataka watu waishi duniani kama wapiti njia, huku akiwahimiza kutenda yaliyo mema kwa kuwa ipo siku watadaiwa hesabu za matendo yao mbele ya Mungu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Askofu Ruwa’ichi ametoa wito huo leo Jumanne, tarehe 24 Agosti 2021, katika Kituo cha Hija cha Pugu, mkoani Dar es Salaam, akihubiri kwenye adhimisho la misa takatifu ya mazishi ya Padri Paul Peter Haule.

“Kila mmoja wetu anayehudhuria adhimisho hili la misa takatifu ni mpita njia, wote tuko wapita njia. Basi tuishi kama wapita njia na wasafiri. Tuishi kama watu ambao siku moja tutadaiwa hesabu ya ukarani wetu,” amesema Askofu Ruwa’ichi.

Askofu Ruwa’ichi ameongeza “tuwe tayari, sababu iko siku Mungu atatutaka tuitoe hesabu ya ukarani wetu na ukarani wetu ni maisha tuliyopewa tuyaishi, ushuhuda tuliyokabidhiwa tuufanye, utume na wajibu tuliokabidhiwa.”

Yuda Thadeus Ruwa’ichi

Padri Haule aliyefariki dunia tarehe 18 Agosti 2021, kwenye Hospitali ya Kardinali Rugambwa, Ukonga, akipatiwa matibabu, alikuwa Paroko Msaidizi wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Petro, Oysterbay mkoani Dar es Salaam.

Akimzungumzia marehemu Padri Haule, Askofu Ruwa’ichi amesema alitumikia nafasi hiyo kwa zaidi ya miaka 20.

“Hayati Paul alianza safari yake ya ufuasi na ushuhuda pale alipobatizwa, akaukumbatia wito wa upadri. Ameishi upadri kwa miaka inayokimbilia, haijafikia 30 lakini inakimbilia huko, tumshukuru Mungu kwa miaka ya upadri aliyomjalia,” amesema Askofu Ruwa’ichi.

Askofu Ruwa’ichi amesema, Padri Haule alijiandaa na safari yake ya kwenda mbinguni, kwa kuwa kabla hajapelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu, alipata sakramenti ya kitubio.

“Padre Paul alijindaa, kabla ya kwenda hospitalini alijiandaa kwa kupokea maskramenti. Sakramenti ya kitubio na sakramenti ya ukaristi, amekimbilia kiti cha huruma ya Mungu na kuomba huruma ya Mungu,” amesema Askofu Ruwa’ichi na kuongeza:

“Akamuomba Mungu aliyemjalia moyo wa kujifahamu na kujiamini sana, amsamehe yale yaliyopungua katika ufuasi na majitolea yake, amjalie mapunziko ya milele pamoja na wateule wake.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!