Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Ruwa’ichi aagiza mapadre wote kuchanjwa
Habari Mchanganyiko

Askofu Ruwa’ichi aagiza mapadre wote kuchanjwa

Yuda Thadeus Ruwa’ichi
Spread the love

 

ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Yuda Thadeus Ruwa’ichi amewaagiza mapadre wote wa jimbo hilo kupata chanjo ya ugonjwa wa corona (COVID-19). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Askofu Ruwa’ichi ametoa wito huo leo Jumanne, tarehe 24 Agosti 2021, katika Kituo cha Hija cha Pugu, jijini Dar es Salaam, wakati akihubiri kwenye adhimisho la misa takatifu ya mazishi ya Padri Paul Peter Haule.

Padri Haule aliyefariki dunia tarehe 18 Agosti 2021, kwenye Hospitali ya Kardinali Rugambwa, Ukonga, akipatiwa matibabu. Alikuwa Paroko Msaidizi wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Petro, Oysterbay mkoani Dar es Salaam.

Kiongozi huyo wa kiroho amesema, tayari Baba Mtakatifu Francis amekwisha kuonesha mfano wa kuchanjwa.

Mwili wa Padri Paul Peter Haule ukiweka kaburini

“Na kwa sababu hiyo, sijui mapadri wangapi ambao mmeshachanjwa, lakini leo naomba nitoe agizo kila Padri akachanjwe, tusifanye utoto, tusifanye lele mama hii Covid-19, haina mjomba na shemeji, inatuumiza,” amesema Askofu huyo

Askofu Ruwa’ichi amewaomba Watanzania wafuate ushauri unaotolewa na wataalamu wa afya, kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.

“Tufuate maelekezo ya wataalamu, najua hiki ni kipindi ambacho kuna maneno mengi.”

“Naomba niwaambie kwamba hata waliotutangulia kuchanjwa ni Baba Mtakatifu Francis, ametupa mfano wa kuchanjwa yeye mwenyewe, mimi nimewapa mfano wa kutangulia kwenda kuchanjwa,” amesema Askofu Ruwa’ichi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!