Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu Mwamakula awachana ACT-Wazalendo kuhusu katiba, yamjibu
Habari za Siasa

Askofu Mwamakula awachana ACT-Wazalendo kuhusu katiba, yamjibu

Kiongozi wa Kanisa la Uamsho la Moravian, Askofu Emmaus Mwamakula
Spread the love

 

KIONGOZI wa Kanisa la Uamsho la Moravian, Askofu Emmaus Mwamakula, amekieleza Chama cha ACT-Wazalendo, kuwa hakiwezi kuingia kwenye uchaguzi bila ya kupatikana Katiba mpya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar ea Salaam … (endelea).

Askofu Mwamakula ametoa kauli hiyo leo Jumamosi, tarehe 29 Januari 2022, katika Mkutano Mkuu Maalumu wa chama hicho, uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar ea Salaam.

Kiongozi huyo wa kiroho amesema kuwa, inabidi Watanzania waungane katika kutafuta katiba moya iliyofanyiwa marekebisho.

“Kuna jambo liko mbele yetu kila mmoja anaongea kwa neno lake, ACT-Wazalendo  siwezi kuwaficha kwenye hili hamuwezi kuingia kwenye uchaguzi na katiba iliyopo. Kama imeshindikana kwa Maalim Seif Shariff Hamad, ambaye alikuwa hanunuliki, msifikiri ninyi mtaweza. Tuungane Watanzania wote katika kutetea kupatikana kwa katiba ambayo haijaandaliwa na mtu mmoja,” amesema Askofu Mwamakula.

Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, amemjibu Askofu Mwamakula akimtaka asiwe na wasiwasi kwani chama hicho kiko tayari kushirikiana na wadau wengine kupigania katiba mpya.

“Usiwe na wasiwasi Askofu, ni ajenda zetu na tutashirkiana na wadu wote wa  mapambano ya kidemokrasia kama tulivyofanya nyakati zote,” amesema Ado.

Ado amesema kipaumbele cha ACT-Wazalendo ni kuhakikisha chaguzi zijazo zinakuwa za haki.

“ACT tulishatamka kupitia kikao kilichoita cha Halmashauri Kuu ya Chama Taifa, ajenda za tume huru ya uchaguzi na katiba mpya ni ajenda  za kipaumbele kwa ACT-Wazalendo.  Tumeyapa hayo kipaumbele sababu tunafahamu mazingira ya kisiasa ya nchi yetu,” amesema Ado na kuongeza:

“Uchaguzi utahitaji tume huru na kwetu sisi tumetamka mwaka 2022 utakuwa mwaka wa kupigania tume huru ya uchaguzi, hatutolala usiku na mchana ili uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 24 na Mkuu wa  2025 uwe na sifa tatu kwanza uwe huru, haki.”

1 Comment

  • Asanten act kwa kumuunga mkono lakini mnaitaji katiba mpya kwa faida gani lifahamishen taifa faida ya katiba mpya .idadi kubwa ya wanachi hata iokatiba ya zamani hawajui faida yake wala hasara yake. Maitaji ya wanachi ni mabadiliko ya maendeleo na walasio katiba mpya kama kweli mnataka katiba mpya anzeni ndani ya act katiba ya act sisi act tumeichoka

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!