Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mauaji Tanzania: Waziri Masauni awaita vigogo wa Polisi
Habari Mchanganyiko

Mauaji Tanzania: Waziri Masauni awaita vigogo wa Polisi

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania, Hamad Masauni akizungumza na makamshna wa Polisi nchini
Spread the love

 

WAZIRI wa Mambo ya Ndani wa Tanzania, Hamad Masauni ameitisha kikao cha watendaji wakuu wa jeshi la Polisi nchini humo ili kupokea na kujadili jinsi ya kudhibiti matukio ya mauaji ya kijamii. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Aidha, Masauni amewataka Polisi kuwasaka na kuwakamata wanaosambaza picha chafu mitandaoni, wanaochafua viongozi na wanaosajilia watu laini za simu.

Masauni ametangaza adhima hiyo leo Jumamosi, tarehe 29 Januari 2022, alipotembelea Kamisheni ya Uchunguzi wa Kisayansi (Forensic Bureau) jijini Dar es Salaam.

Masauni aliyepanda wadhifa na kuwa wiziri wa wizara hiyohiyo hivi karibuni kwa kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, ameitisha kikao hicho, ofisini kwake jijini Dodoma keshokutwa- Jumatatu tarehe 31 Januari 2022.

Waziri huyo ametoa ameitisha kikao hicho ikiwa ni siku nne, tangu Makamu wa Rais wa Tanza ia, Dk. Philip Mpango kutoa siku saba kwa Inspekta Jenerali wa Polisi – IGP Simon Sirro kuwakamata watuhumiwa wa matukio ya mauaji pamoja na kukomesha matukio hayo.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania, Hamad Masauni

Dk. Mpango alitoa agizo hil tarehe 26 Januari, 2022 alipotembelea wafiwa wa ndugu wa marehemu watano wa familia moja waliofungiwa ndani na kuuawa, lilitokea hivi karibuni katika kijiji cha Zanka wilayani Bahi Mkoa wa Dodoma.

“Nimefika hapa kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan kuja kutoa pole kwa familia ambayo imetendewa ukatili huu, lakini kutoa pole kwa kijiji cha Zanka na vijiji vyote vya jirani… poleni sana.

Makamu huyo wa Rais alisema,”Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Dodoma, nifikishie salam kwa IGP, mauaji haya nchi nzima yakome, mfanye kazi ya kuyazuia, polisi mna kazi kubwa ya kufanya nchini. Rais Samia na mimi tumechoka hatuwezi kuongoza nchi yenye mauaji namna hii.”

Maagizo hayo ya Dk. Mpango anayatoa kipindi ambacho kumekuwapo na ongezeko la mauaji ya wananchi ama kunyongwa, kujinyonga na au kuuawa katika maeneo mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!