Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Ajali ya moto Moro: Vifo vyaongezeka
Habari Mchanganyiko

Ajali ya moto Moro: Vifo vyaongezeka

Spread the love

MAJERUHI saba kati ya 32 waliokuwa wakiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), wamefariki dunia usiku wa kumkia leo tarehe 15 Agosti 2019. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Idadi ya majeruhi waliopokewa MNH baada ya kutokea ajali ya moto mkoani Morogoro tarehe 10 Agosti 2019, walikuwa 46 ambapo mpaka sasa hospitalini hapo majeruhi 21 wamepoteza maisha.

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 15 Agosti 2019, Meneja Uhusiano wa MNH, Aminiel Aligaisha amesema majeruhi saba wamefariki dunia kuanzia majira ya usiku hadi asubuhi ya leo.

Aligaisha ameeleza kuwa, kwa sasa majeruhi wamebakia 25 ambapo 16 kati yao wako kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) huku tisa wakiwa katika wodi ya Sewahaji.

“Tulipokea wagonjwa 46 idadi ya vifo ilikua 14 mpaka jana nilipozungumza na ninyi saa tano na nusu, nasikitika kutangaza kwamba hadi leo, wameongeza wengine 7 na kufikia idadi ya 21 mpaka sasa, kati ya wgaonjwa 46 tulipopokea wamefariki 21 na tumebaki na 25 na kati yake 16 wako ICU  na 9 wako katika wodi ya Sewahaji,” amesema Aligaisha .

Aligaisha amesema madaktari na wauguzi wanaendelea na juhudi za kuokoa maisha ya majeruhi waliobakia.

“Tunaendelea na jitihada za kutibu wagonjwa wengine. Madaktari na wauguzi wanafanya jitihada kuhakikisha majeruhi wanahudumiwa vizuri,” amesema Kebwe.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Stephen Kebwe amesema leo anatarajia kutoa idadi kamili ya vifo vya majeruhi hao, baada ya kuwepo kwa takwimu zinazotofautiana kuhusu idadi ya vifo hivyo.

Aidha, Kebwe amesema mpaka jana tarehe 14 Agosti 2019 idadi ya vifo hivyo ilikuwa 85, baada ya majeruhi wengine 14 waliolazwa MNH kufariki dunia.

Ajali hiyo ilitokea majira ya asubuhi tarehe 10 Agosti 2019 eneo la Msamvu mkoani Morogoro, baada ya tenki la lori la mafuta aina ya petrol kulipuka kufuatia baadhi ya wananchi kutoboa tenki la lori hilo na kuanza kuchota mafuta.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!