Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shughuli pevu: Ni Lissu Vs Ndugai kortini
Habari za SiasaTangulizi

Shughuli pevu: Ni Lissu Vs Ndugai kortini

Spread the love

KESI inayotarajiwa kuwa mashuhuri na ya aina yake kati ya Tundu Lissu, aliyevuliwa ubunge wa Jimbo la Singida Mashariki dhidi ya Job Ndugai, Spika wa Bunge, sasa kuunguruma. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea). 

Kesi hiyo inatarajiwa kuanza leo tarehe 15 Agosti 2019, katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam Lissu akipinga uamuzi wa Spika Ndugai kumvua ubunge.

Lissu, mmoja wanasheria mashuhuri nchini, alifungua shauri la kupinga kuvuliwa ubunge wake, kwenye mahakama hiyo Jumatano, tarehe 7 Agosti 2019, chini ya hati ya dharura.

“Maombi ya kesi hii yatasikilizwa mbele ya Jaji Mtupa. Hati ya wito wa mahakama inabainisha kuwa mlalamikiwa ambaye ni Spika Ndugai, atatakiwa kufika mahakamani bila kukosa,”

imeeleza taarifa ya Tumaini Makene, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Chadema na kuongeza;

“Tunatoa wito kwa viongozi, wanachama, wafuasi wa Chadema na Watanzania wote wapenda haki, demokrasia na utawala bora unaoheshimu sheria, mahali popote walipo kufuatilia kwa karibu mwenendo wa shauri hilo kuanzia hatua ya sasa.”

Spika Ndugai alitangaza uamuzi wa kumvua ubunge Lissu, tarehe 28 Juni 2019, wakati akiahirisha mkutano wa 15 wa Bunge. Hatua hiyo iliibua sintofahamu na kupingwa.

Kiongozi huyo wa Bunge, alitaja sababu za kumvua ubunge Lissu kuwa: Kushindwa  kuhudhuria vikao vya bunge bila kutoa taarifa kwa maandishi kwa spika na kutojaza fomu ya taarifa za mali na madeni kwa mujibu wa sheria ya maadili ya viongozi wa umma ya mwaka 1985.

Lissu kupitia kaka yake, Alute Mughwai, anaomba Mahakama Kuu imruhusu kufungua shauri la kupinga kuvuliwa ubunge wake, kupitia utaratibu wa Judicial Review – mapitio ya maamuzi yaliyofikiwa.

Lakini pia Lissu anaiomba mahakama itoe amri ya muda ya kusimamisha kuapishwa kwa mbunge mteule wa jimbo la Singida Mashariki (CCM), Miraji Mtaturu.

Lissu anaiomba mahakama isikilize na kutoa uamuzi wa maombi yake haraka, vinginevyo Mtaturu ataapishwa kushika wadhifa huo, na kwamba, hatua yoyote ya kutosikiliza shauri lake kwa haraka, litamuathiri moja kwa moja kwa kuwa amepoteza haki zake zote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!