KAMATI Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo imeazimia kuwasilisha kwa Maakmu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Rais wa Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Nakala ya barua hiyo pia itawasilishwa kwa kwa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Samia Suluhu Hassan.
Hayo yamebainishwa leo Jumapili tarehe 22 Januari, 2023 na Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maazimio ya Kamati Kuu ya chama hicho iliyoketi jana makao makuu ya chama hicho.
Pia chama hicho kimeonesha nia ya kuonana na mabalozi wanaozikilisha nchi zao hapa nchini ili kuwaleza mwenendo usioridghisha wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.
Shaibu amesema awali chama hicho kilipokea taarifa kutoka kwa wawakilishi wa Jumuiya ya Kimataifa kuwa Mataifa na Mashirika ya Kimataifa yamerejesha mahusiano mazuri na Zanzibar kutokana na uwepo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa.
“Kamati Kuu imewaagiza viongozi wakuu wa Chama kuonana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na serikali zao kuwaeleza mwenendo wa sasa usioridhisha wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar,” amesema Shaibu.
Mbali na kumwandikia barua pia chama hicho kimemtaka Rais Dk. Mwinyi kuweka wazi Ripoti ya Kikosi Kazi alichokiunda kushughulikia masuala ya demokrasia Zanzibar.
Shaibu amesema Dk. Mwinyi anapaswa kuiga mfano wa mwenzake Rais Samia Suluhu Hassan ambaye Ripoti ya Kikosi Kazi hake imewekwa wazi kwa umma na inapatikana kwenye tovuti.
“Penye nia ya dhati, masuala yanayogusa maslahi ya umma huwekwa wazi. Hakuna sababu inayohalalisha kufichwa kwa Ripoti ya Kikosi Kazi Zanzibar,” amesema Shaibu.
Shaibu ameongeza kuwa Kamati Kuu imeweka muda wa utekelezwaji wa makubaliano baina ya Rais Mwinyi na Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad waliyoyafanya kabla ya ACT Wazalendo kuingia kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa.
Amezitaja hoja hizo kuwa ni kufanyika uchunguzi huru wa kimahakama kuhusu uvunjwaji wa haki za binadamu wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 na kuwapatia fidia wahanga wa uchaguzi huo na kufanyiwa mapitio na mabadiliko mfumo wa uchaguzi na Mahakama wa Zanzibar.
Amesema kuwa kwenye vikao mbalimbali Rais Mwinyi amekuwa akieleza kuwa hoja za maridhiano zitatekelezwa kwa ufanisi atakapochaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM.
“Tunataka utekelezaji kwa vitendo wa Hoja Tatu zilizowasilishwa kwa Rais Mwinyi,” amesisitiza Shaibu.
Amesema hadi sasa hoja iliyofanyiwa kazi ni ya kuachiwa huru viongozi wa ACT Wazalendo waliokuwa mahabusu au wameshikiliwa kwa njia nyingine.
Leave a comment