Tuesday , 21 May 2024
Home Kitengo Biashara TPA yakamilisha mifumo ya TEHAMA, ikiwa ni utekekezaji wa maagizo ya Rais Samia
Biashara

TPA yakamilisha mifumo ya TEHAMA, ikiwa ni utekekezaji wa maagizo ya Rais Samia

Spread the love

 

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), chini ya Mkurugenzi Mkuu, Plasduce Mbossa imefanikiwa kutekeleza kwa mafanikio makubwa maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kuwa na mifumo Madhubuti ya Tehama inafanya kazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salam … (endelea).

Katika mwaka wa fedha 2022/2023 miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana ikiwa pia ni Pamoja na utekelezaji wa maagizo ya Rais ni kama ifuatavyo;

  • Kukamilika kwa asilimia kubwa mradi wa TEHAMA (Enterprise Resource Planning, ERP) ambao hutumika katika kuandaa na kuhifadhi taarifa za kifedha na kuunganisha shughuli za Idara mbalimbali katika kutekeleza majukumu ya kila siku. Mfumo huo unaunganisha Idara zote muhimu kwa mfano Idara ya Fedha, Idara ya Rasilimali watu, Idara ya manunuzi na nyingine.
  • Matokeo ya kukamilika kwa mfumo huo, ni sambamba na ufanisi katika uandaaji na utoaji wa taarifa za hesabu za Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania, ambapo mfumo huo umeiwezesha TPA kupata hati safi kwa miaka miwili mfululizo kwa kaguzi zinazofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).
  • Aidha, kutokana na matumizi ya mfumo huo, TPA imeweza kupata tuzo ya uandaaji bora wa taarifa za hesabu kutoka kwa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu, NBAA.
  • Zaidi ya hayo, mfumo huo umeongeza tija pia katika kuhakikisha udhibiti wa mianya ya upotevu wa fedha, uandaaji wa taarifa mbalimbali kwa wakati, utunzaji wa nyaraka na taarifa za kifedha na rasilimali za taasisi. Kutokana na kuimarika mifumo ya ukusanyaji mapato imepelekea mapato ya TPA kuongezeka kwa asilimia 27 kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ikilinganishwa na mwaka wa fedha 2021/2022.
  • Mafanikio mengine ni kwa upande wa kuhudumia shehena ambapo kumekua na ongezeko kubwa kwa upande wa Meli na shehena ambapo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 idadi ya Meli zilizohudumiwa na Bandari za TPA ziliongezeka na kufikia meli 4,762 kutoka meli 4,160 ambazo ni wastani wa ongezeko la asilimia 13.9 kwa mwaka.
  • Kwa upande wa shehena kiwango cha shehena kilichohudumiwa ni tani milioni 8 sawa na wastani wa ongezeko la asilimia 21.7 ya shehena iliyohudumiwa katika mwaka husika ukilinganisha na miaka ya nyuma.
  • Aidha kwa upande wa miundombinu, Mamlaka ya bandari imefanya uboreshaji mkubwa wa miundombinu ikiwemo uundwaji wa mifumo ya TEHAMA, Utekelezaji wa Mradi wa Kimkakati wa Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam (DMGP), Uboreshaji wa Bandari Tanga, Upanuzi wa Bandari ya Mtwara, Uboreshaji wa Bandari za Maziwa Makuu
  • Uwekezaji huo mkubwa na ununuzi wa mitambo pamoja na ujuzi kwa wafanyakazi umeongeza ufanisi wa utendaji kazi kwa Mamlaka ya Bandari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

Benki ya Exim yazindua huduma ya ‘Exim Smart Shule’

Spread the love  KATIKA juhudi za kuboresha teknolojia za kidijitali katika sekta...

Biashara

Shinda mkwanja Meridianbet Kasino, ukicheza Expanse Tournament.

Spread the love  LION Kingdom ni sloti kutoka kasino ya mtandaoni yenye...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yapata idhini kuwa wakala wa madalali wa DSE

Spread the loveBenki ya NMB imepata idhini kutoka Benki Kuu ya Tanzania...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Waziri aipongeza NBS kwa mafanikio

Spread the loveNaibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande amepongeza Ofisi ya Taifa...

error: Content is protected !!