Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CUF: ACT inakurupuka kujitoa SUK
Habari za Siasa

CUF: ACT inakurupuka kujitoa SUK

Maftaha Nachuma
Spread the love

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Maftaha Nachuma amesema kuwa Serikali ya umoja wa Kitaifa (SUK)-imetokana na maridhiano ya chama chao (CUF) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo Chama cha ACT-Wazalendo hakijui misingi yake ndio maana kinakurupuka kutaka kujitoa. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Nachuma ameyasema hayo jana tarehe 14 Machi 2024, wakati akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam na kueleza kuwa SUK haikuundwa kukinufaisha chama cha siasa isipokuwa imeanzishwa kwa maslahi ya wananchi wa Zanzibar.

” “Hakuna chama kilichopitia magumu kama Chama cha Wanachi -CUF, sisi ndio chama ambacho watu wake wengi waliuawa mwaka 2001 hadi Rais mstaafu Hayati Benjamini Mkapa akaelezea kujutia kwa mauaji hayo ndio maana nasema hawa wanaojitoa SUK hawajui misingi ya SUK,” amesema Nachuma.

Amesema kuwa msingi wa kuundwa kwa serikali ya umoja unatokana na kuchoshwa na matukio ya umwagaji damu za wanachi na kuunganisha mawazo ya Wazanzibar wote kwenye serikali.

“Tunafahamu bado kuna matatizo ndani ya Serikali ya CCM lakini sio suala la kujitoa kwenye SUK kwa sababu rahisi rahisi tu” amesema Nachuma.

1 Comment

  • Nachuma, umeongea. Tunashangaa huyu ACT Makamu wa Rais, baada ya kwenda mbele anaturudisha kusiko.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!