Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Mongela awaaga 818 wanaohama Ngorongoro
Habari za Siasa

RC Mongela awaaga 818 wanaohama Ngorongoro

Spread the love

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella amewahakikishia wananchi wanaohama kwa hiari kutoka ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kwenda maeneo mengine nje ya hifadhi kuwa serikali imejipanga na hakuna mwananchi yoyote atakayekosa haki zake iwapo ataamua kuhama kwa hiyari. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mongella ametoa kauli hiyo wilayani Ngorongoro mkoani Arusha leo tarehe 25 Januari, 2024 wakati akiwaaga wananchi 818 walioamua kuhama kwa hiyari kutoka ndani ya hifadhi hiyo na kwenda kuishi katika Kijiji cha Msomera wilayani Handeni Mkoani Tanga.

Ameeleza kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha za kutosha ili kuhakikisha kuwa zoezi hilo linafanikiwa na hakuna mwananchi yoyote atakayekosa kulipwa haki zake zote zilizoanishiwa katika utekelezaji wa zoezi hilo.

Mkuu wa Mkoa ameongeza kuwa zoezi hilo linatekelezwa kwa kuzingatia misingi yote ya haki za binadamu ikiwemo kuboresha maisha ya wananchi hao wanapofika katika Kijiji cha Msomera wilayani Handeni mkoani Tanga.

Kwa upande wake Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Richard Kiiza amesema kumekuwa na muamko na ari kubwa ya wananchi kujiandikisha na kutaka kuhama kwa hiyari ambapo  katika  tukio hilo jumla ya kaya 118 zenye watu  818 na mifugo  3,129 wamehama kwenda Kijiji cha Msomera.

Mratibu wa zoezi hilo la kuhamisha watu kutoka Hifadhi ya Ngorongoro, Fedes Mdalla amesema uhamisishaji wa wananchi kuhama ndani ya hifadhi unaendelea na zoezi hilo litakuwa linafanyika kila mara kulingana na idadi ya nyumba zinazoendelea kujengwa na kukamilika katika eneo la mradi.

Baadhi ya wananchi walioamua kuhama kwa hiyari kwenda katika Kijiji hicho wameishukuru serikali kutokana na jinsi inavyozingatia utu na maslahi ya kila mmoja katika kuhakikisha kuwa wanapata stahiki zao.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao Sindato Ngenyike na Theresia Moko wamesema kitendo cha wao kuondoka ndani ya hifadhi kimetokana na elimu waliyoipata  kutoka kwa serikali na wananchi wenzao ambao tayari wameshamia katika Kijiji cha Msomera.

Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro inaendelea kuelimisha, kuandikisha na kuhamisha wananchi kutoka ndani ya hifadhi hiyo kila wiki ikiwa ni zoezi lenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi na pia kulinda na kuimarisha hifadhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!