Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Samia amtumbua mkurugenzi Dart
Habari MchanganyikoTangulizi

Samia amtumbua mkurugenzi Dart

Spread the love

Hatimaye Rais Samia Suluhu Hassan  ametengua uteuzi wa Dk. Edwin P. Mhede aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi yaendayo Haraka (DART). Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).


Dk. Mhede ambaye imeelezwa atapangiwa kazi nyingine, nafasi yake imechukuliwa na Dk. Athuman Kihamia aliyewahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha.

Hatua hiyo inajiri baada ya kuzorota kwa muda mrefu kwa huduma za usafiri wa mabasi hayo jijini Dar es Salaam na kuzidisha adha ya usafiri kwa wakazi wa jiji hilo huku uongozi wa  Dart ukiendelea kukaa kimya bila kuchukua hatua zozote.

Aidha, taarifa iliyotolewa leo Alhamisi na Mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunus pia Rais Samia amemteua Musa N. Kuji kuwa Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA). Kuji alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!