Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge agawa mitungi 107 kwa makada wa CCM Ileje
Habari za Siasa

Mbunge agawa mitungi 107 kwa makada wa CCM Ileje

Spread the love

Mbunge wa Ileje ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya amekabidhi mitungi 107 kwa wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM wilayani humo ukiwa ni mwendelezo wa kuhamasisha kampeni ya uhifadhi wa mazingira. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Kasekenya amekabidhi mitungi hiyo kwa wajumbe hao leo tarehe 2 Januari 2024 katika makundi mawili ambapo kundi la kwanza ni wajumbe wa tarafa ya Bundali ambapo zoezi hilo limefanyika katika ofisi za wakala wa misitu Tanzania wilaya ya Ileje (TFS) na kundi la pili limewakutanisha wajumbe wa halmashauri kuu CCM wilayani humo katika ofisi za chama hicho zilizopo Itumba.

Amesema mitungi hiyo itakuwa mwanzo kwa wajumbe wa halmashauri ya wilaya ili wawe chachu ya darasa kwa wananchi wa Ileje kupambama na tatizo la mabadiliko ya tabia nchi.

Ameeleza kuwa matumizi ya gesi hiyo yatasaidia ufanisi kwa akina mama kulinda mazingira na kujiepusha na matumizi ya mkaa.

“Wajumbe hawa watakuwa chachu ya kuleta mabadiliko ya uoto wa asili kutokana na uharibifu wa mazingira kwa ajili ya matumizi ya kuni kwa ajili ya kupikia lakini mitungi hii itaenda kuwa mwarobaini kusaidia  mazingira ya Ileje,” amesema.

Amesema ugawaji wa mitungi hiyo 107 ni mwanzo kwani ajenda ya kitaifa ni kupambana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo imesababishwa na uharibifu wa mazingira hivyo itakuwa ni mwendelezo kwa makundi mengine.

“Niwahimize wananchi wote wenye kipato kuondokana na matumizi ya kuni na kwenda kwenye matumizi ya gesi kama ilivyo ajenda ya kitaifa ya kukabiliana na manadiliko ya uoto wa asili,” amesema.

Mbunge huyo ambaye amekuwa akipambana kutatua changamoto za jamii, amewashauri wajumbe hao na  wadau wengine kumuunga mkono kufanikisha Kampeni ya Pika kwa Gesi, Tunza Mazingira.

Pia amesema kufikia makundi mengine kwenye jamii kwa lengo la kulinda afya za akina mama, kutunza mazingira na kuepusha madhara ya mabadiliko ya tabia nchi, mambo ambayo yatapelekea kuimarisha lishe bora.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!