Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the love

WAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amewataka watanzania kuongeza jitihada za kuleta maendeleo pamoja na kukemea ubaguzi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Mbowe ametoa wito huo leo tarehe 9 Disemba 2023, kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii. Tanganyika huadhimisha siku ya uhuru tarehe 9 Disemba kila mwaka.

“Tunapoadhimisha, naomba tujenge upya mioyo yetu na kuahidi kuwa jasiri tena katika harakati zetu za maendeleo na ustawi. Naomba tuwe hodari katika jitihada zetu za kujenga Tanzania inayojumuisha kila mmoja wetu bila ubaguzi, yenye haki kwa kila mmoja wetu, na yenye neema kwa wote,” ameandika Mbowe.

Mwenyekiti huyo wa Chadema amesema licha ya mafanikio mbalimbali ambayo Tanganyika imepata tangu uhuru, lakini bado inakabiliwa na janga la umasikini kwa watu wake.

“Tunaadhimisha miaka 62 ya uhuru tukikumbuka pia umasikini wa watu wetu katikati ya wingi wa rasilimali, fursa zilizopotea na ahadi zilizovunjwa kutokana na sera na uongozi ambao haukutumia nguvu na ujasiri wa Watanzania,” ameandika Mbowe.

Amewataka Watanzania waenzi juhudi za waliopigania uhuru kwa kulipigania taifa kwa ujasiri pamoja na kukataa ahadi alizoita za uongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!