Saturday , 18 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea
Habari Mchanganyiko

Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea

Spread the love

MAWASILIANO ya barabara ya Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam, kupitia Bagamoyo, yaliyokuwa yamefungwa baada ya sehemu ya Daraja la Mto Mpiji kumomonyoka uliosabaishwa na mvua za El-Nino, yamerejeshwa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Uhusiano cha Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mawasiliano hayo yamerejeshwa asubuhi ya leo tarehe 9 Disemba 2023, baada ya barabara hiyo kufungwa jioni ya jana Ijumaa.

Taarifa ya wakala huo ilisema, daraja hilo lilifungwa kwa ajili ya usalama wa wasafiri na kwamba limefunguliwa baada ya watalaamu wake kufanya jitihada za kutengeneza hitilafu iliyojitokeza.

“TANROADS imerejesha mawasiliano ya barabara ya mikoa ya Pwani na Dar es Salaam, kupitia Bagamoyo baada ya daraja la Mpiji linalounganisha mikoa hiyo kupata changamoto ya kumomonyoka kutokana namvua za El-Nino,” imesema taarifa hiyo na kuongeza:

“TANROADS imeruhusu watumiaji wa barabara hiyo kupita upande mmoja wa daraja baada ya matengenezo kukamilika, huku timu ya watalaamu na mkandarasi wakiendelea kufanya matengenezo mengine ya haraka kulirejesha kwenye hali yake ya awali na kulifanya liweze kuwa na uimara zaidi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua bima ya afya kwa wakulima

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na kampuni...

Habari Mchanganyiko

Makamba awasili China kwa ziara ya kikazi

Spread the loveWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Ethiopia yafungua njia ujenzi wa ubalozi Dodoma

Spread the loveSerikali ya Tanzania imeipongeza Serikali ya Ethiopia kwa kuweka historia...

error: Content is protected !!