Tuesday , 21 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT Wazalendo washtushwa vifo 47 mafuriko Hanang
Habari za SiasaTangulizi

ACT Wazalendo washtushwa vifo 47 mafuriko Hanang

Spread the love

CHAMA cha ACT Wazalendo kimeelezza kupokea kwa mshtuko na simanzi kubwa taarifa za vifo vya watu 47 na majeruhi 85 vilivyotokea wilayani Hanang mkoani Manyara kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika mikoa mbalimbali nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu na Naibu Katibu Mwenezi wa ACT Wazalendo, Janeth Rithe imesema wanatoa pole na salaam za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote kwa maafa haya makubwa yaliyotokea huku tukiwaombea kwa Mwenyezi Mungu majeruhi waweze kupona haraka na kuendelea na maisha yao ya kila siku.

Aidha, kutokana na maafa haya mazito, tunatoa wito kwa Serikali kuhakikisha majeruhi wanapata huduma zote stahiki zinazohitajika, huduma za kibinadamu kwa wakazi wote wa maeneo yaliyoathirika na maafa hayo sambamba na kukarabati miundombinu mbalimbali iliyoharibika kwa haraka zaidi.

Vifo hivyo na majeruhi hao wametokana na mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia jana Jumapili tarehe 3 Desemba 2023 baada ya sehemu ya Mlima Hanang kumomonyoka na kusababisha tope kutiririka katika makazi ya watu wa maeneo ya Katesh na Gendabi wilayani humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaKimataifaTangulizi

Waliowekewa damu yenye VVU, homa ya ini kulipwa fidia trilioni 32.9

Spread the loveWaziri mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak ameahidi kulipa fidia ya...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yanawa mikono fidia Kimara-Kibamba

Spread the loveSERIKALI imewataka waathiriwa wa bomoabomoa ya upanuzi wa barabara ya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Geita, Mwanza waongoza kwa mbwa

Spread the loveNaibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Alexander Mnyeti amesema taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 25,039, taasisi 65 wahamia Dodoma

Spread the loveSerikali imesema hadi sasa, jumla ya watumishi 25,039 kutoka Serikali...

error: Content is protected !!