Friday , 17 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Aliyehitimu udaktari HKMU na miaka 21 atoa siri
Elimu

Aliyehitimu udaktari HKMU na miaka 21 atoa siri

Spread the love
MHITIMU wa fani ya udaktari ambaye ni mdogo kuwahi kutokea tangu kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert kairuki (HKMU), Ahlam Azam Mohamed, ametoa siri ya namna alivyofanikiwa kuhitimu akiwa na miaka 21. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Akizungumza na Nipashe jana mara baada ya mahafali ya 21 ya chuo hicho, Mikocheni jijini Dar es Salaam, Ahlam alisema alimaliza darasa la saba akiwa na umri wa miaka 13 na baada ya hapo hakuendelea na masomo ya darasani.

Alisema baba yake alikuwa akimletea walimu wa masomo mbalimbali nyumbani ambao walimfundisha kwa miezi hiyo minne na kumudu kufanya mtihani wa kidato cha nne katika shule ya Almuntazir kama mtahiniwa binafsi.

“Nilisomea nyumbani masomo ya sekondari ya kidato cha kwanza hadi cha nne kwa miezi minne kisha kikasoma masomo ya kidato cha tano na sita ndani ya mwaka mmoja kwa hiyo nilimaliza masomo ya kidato cha sita nikiwa na miaka 15,” alisema

“Nilijaribu kujiunga na vyuo lakini majibu yalichelewa kwa hiyo nikalazimika kusubiri mwaka mzima nikaja kujiunga na masomo ya udaktari hapa Kairuki mwaka 2018 nikiwa na miaka 16 na nafurahi leo hii nimehitimu udaktari,” alisema

Alisema alivutiwa kusomea nyumbani baada ya kumuona  kaka yake amefanikiwa kusoma masomo hayo ya kidato kwanza hadi cha nne akiwa nyumbani na kufaulu kwenye mitihani yake.

Awali, Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Yohana Mashalla, alisema chuo kinaona fahari kwa mara ya kwanza kuwa na mhitimu mdogo wa fani ya udaktari kuwahi kutokea tangu kuanzishwa kwa chuo hicho.

Alisema mhitimu huyo Alham Azam Mohamed alijiunga na chuo hicho mwaka 2018 ambapo amekuwa akifanya vizuri zaidi kwenye masomo yake yote na kufanikiwa kupata Shahada ya udaktari.

“Tulijaribu kupekua pekua kwenye maeneo mbalimbali nchini kuangalia kama kwenye vyuo vya wenzetu hapa nchini kuliwahi kuwa na mhitimu wa fani ya udaktari mwenye umri kama huu lakini ilionekana kwamba mbali na HKMU,  hapa nchini huyu ni wa kwanza,” alisema

Kwenye mahafali hayo, wahitimu walikuwa 308 ambapo mhitimu mmoja alitunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Sayansi yaani Doctor of Science (Honoris Cause), 13 Stashahada ya Ustawi wa Jamii, 82 Stashahada ya Uuguzi, 14 Shahada ya Ustawi wa Jamii, 35 Shahada ya Uuguzi, 150 Shahada ya Udaktari wa Binadamu.

Wahitimu wawili walitunukiwa Shahada ya Uzamili ya udaktari wa binadamu katika tiba ya afya ya watoto, watatu Shahada ya Uzamili ya Upasuaji, watatu Shahada ya Uzamili ya Magonjwa ya wanawake na uzazi na sita Shahada ya Uzamili ya Tiba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Waziri SMZ akoshwa na kazi za Global Education Link

Spread the loveSERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar SMZ imesema itaendesha msako na kuzifutia...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

error: Content is protected !!