Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wawili mbaroni tuhuma za kumuua mlinzi wa baa
Habari Mchanganyiko

Polisi wawili mbaroni tuhuma za kumuua mlinzi wa baa

Spread the love

ASKARI wawili wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, wanashikiliwa kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga risasi aliyekuwa mlinzi wa baa moja iliyoko maeneo ya Sinza, jijini humo, inayofahamika kwa jina la Board Room. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana tarehe 29 Novemba 2023 na Kaimu Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, ACP G.J Puppa, askari hao wanadaiwa kutekeleza tukio hilo usiku wa kuamkia jana, baada ya mkujeruhi mlinzi huyo, Razaki Azan, kwa risasi.

Taarifa hiyo imesema kuwa, mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, kwa ajili ya kukamilisha uchunguzi.

“Jeshi la Polisi lilipokea taarifa kuwa, askari wawili majira ya Saa sita usiku walimjeruhi mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Razaki Azan mwenye umri wa miaka 29, mlinzi binafsi wa baa ya Board Room, ambaye baadae alipoteza maisha,” imesema taarifa hiyo na kuongeza:

“Jeshi la Polisi tayari limewakamata askari hao na mambo ya kisheria yanakamilishwa na watachukuliwa hatua za kisheria haraka kadri iwezekanavyo kwa kufuata mifumo ya kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!