Monday , 20 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mchungaji USA: Watanzania fanyeni kazi, miujiza ya mafuta, maji ni ulaghai
Habari Mchanganyiko

Mchungaji USA: Watanzania fanyeni kazi, miujiza ya mafuta, maji ni ulaghai

Spread the love

JAMII imetakiwa kufanya kazi ambazo zitawaingizia kipato kwa ajili ya kuinua uchumi wao badala ya kujenga fikra ya kupata miujiza kwa kununua udogo, maji au mafuta kutoka kwa manabii. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Hayo yameelezwa na Mchungaji Prof. Livingston Imbuga wakati akizungumza na waumini wa Kanisa la PAG lililopo Sabasaba Jijini Dodoma katika hafla fupi ya kumtunuku shahada ya uzamivu ya heshima, Mchungaji Charles Kanyika.

Mchungaji Charles Kanyika

Prof. Imbuga ambaye pia ni mwalimu wa Chuo kikuu cha International Universty of Ministry and Education Missouri  cha nchini Marekani, amesema watu wengi wavivu kufanya kazi na hawana uelewa wa kutosha kuhusu neno la Mungu hali inayowalazimu kutegemea zaidi miujiza kutoka kwa manabii ambao kwa kiasi kikubwa ni wachumia tumbo.

Amesema wapo watu ambao wanajiita mitume na manabii ambao wanacheza na akili za watu kuwa kuwauzia vitu ambavyo haviwezi kuwasaidia badala ya kuwafundisha kufanya kazi kwa lengo la kujipatia kipato.

Amesema kuwa mtu hawezi kuwa na uchumi imara kama hafanyi kazi kwa bidii kwani Mungu anaeleza bayana kuwa asiyefanya kazi na asile na kuongeza atabariki kazi za mikono na si kununua udogo au mafuta na maji.

Kwa upande wake Mchungaji wa kanisa la PAG, Dk. Charles Kanyika baada ya kutunukiwa PhD ya heshima ya utatuzi wa migogoro na kuhudumia jamii, amesema kati ya jambo ambalo hakubaliani nalo ni kuona watu wanaonewa au wananyanyaswa.

Amesema kwa kipindi hiki ambacho Tanzanian inaelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na uchaguzi mkuu 2025, haki ni lazima itendeke na asiwepo mtu wa kumuonea mwenzake.

Mchungaji Prof. Livingston Imbuga

Amesema ili kuwa na amani ni lazima kuwepo haki na haki pekee ndiyo inayoweza kuzalisha amani  kwa kuwasikiliza wananchi na kuwaacha wachague mtu ambaye wanamuamini.

Aidha, amewataka viongozi wote kwa kada mbalimbali kuhakikisha wanatenda haki huku akiwakumbusha viongozi wa dini kusimama kidete kuhubiri haki, amani na upendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 85,471 walioenguliwa kipindi cha JPM wapandishwa vyeo

Spread the loveSERIKALI imesema kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa jumla...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

error: Content is protected !!