Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Wanafunzi waliofanya mtihani wakiwa na watoto wachanga wamkuna Jokate
ElimuHabari za Siasa

Wanafunzi waliofanya mtihani wakiwa na watoto wachanga wamkuna Jokate

Spread the love

KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake Tanzani (UWT), Jokate Mwegelo amesema hatua ya wanafunzi walioruhusiwa kufanya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2023 huku wakiwa na watoto wachanga, ni uamuzi wa kipekee ambao umefufua ndoto za mabinti hao. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Amesema uamuzi huo ambao uliasisiwa na Rais Samia Suluhu Hassan, umelenga katika kuhakikisha kila mwanafunzi anatimiza ndoto yake kupitia elimu.

Joketi ametoa kauli hiyo leo Jumamosi alipotembelea eneo la Chamazi Magengeni Jijini Dar es salaam na kukutana na binti aliyefanya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2023 huku akiwa ananyonyesha.

Mbali na binti huyo, pia Jokate amekutana na binti mwingine anayeishi maeneo ya Mbande Jijini Dar es salaam ambaye na yeye amefanya mitihani huku akiwa ananyonyesha mtoto mwenye siku nane.

Aidha, mbali na kuwapongeza kwa jitihada za kufanya mtihani huo, Joketi pia ametoa wito kwa wazazi kuzingatia malezi bora ya watoto ili kuwaepusha na mimba za utotoni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!