Saturday , 18 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ataka udhibiti utitiri wa makanisha yenye mafundisho mabovu
Habari za Siasa

Mbunge ataka udhibiti utitiri wa makanisha yenye mafundisho mabovu

Kilumbe Ng’enda
Spread the love

MBUNGE wa Kigoma Mjini, Kilumbe Ng’enda (CCM) ameiomba  Serikali iweke mkazo katika usajili wa makanisa na taasisi za dini za madhehebu mbalimbali, ili kudhibiti yanayodaiwa kufundisha imani zenye madhara kwa jamii. Anaripoti Jemimah Samwel…(endelea).

Akizungumza katika kipindi cha maswali na majibu, bungeni jijini Dodoma, leo tarehe 7 Novemba 2023, Ng’enda alidai kumekuwa na utitiri wa makanisa na taasisi nyingi za dini, kutokana na kukosekana kwa udhibiti katika usajiri wake.

“Serikali inapaswa kuweka usajili katika taasisi na madhehebu ya dini, hiyo itasaidia kupunguza madhara yanayoletwa na taasisi hizo,” amesema Ngenda.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Jumanne Sagini amesema usajili wa taasisi hizo unafanywa kupitia Ofisi ya Msajili wa Jumuiya na kwamba kabla hazijasajiliwa hupitiwa ili kubaini kama zimekidhi vigezo.

“Ofisi ya Msajili inaendelea kushughulikia maombi ya usajili wa taasisi na madhehebu ya dini na kutoa usajili kwa wakati kwa taasisi zenye sifa stahiki. Lakini kuhakikisha Serikali haisajili taasisi  ambazo zinaweza kuleta madhara kwa jamii na kuhamasisha vitendo ambavyo ni kinyume na mila na maadili ya kitanzania,” amesema Sagini.

Sagini, amesema jumla ya maombi ya usajili wa taasisi na madhehebu ya dini 1,858 yalipokelewa katika Ofisi ya Msajili wa Jumuiya, ambapo taasisi 419 zilisajiliwa, wakati maombi ya taasisi nne yakikataliwa huku maombi 1,435 yakiwa katika hatua mbalimbali za usajili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!