Friday , 17 May 2024
Home Kitengo Biashara Serikali kununua mitambo 15 ya kuchoronga miamba
BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kununua mitambo 15 ya kuchoronga miamba

Spread the love

Serikali kupitia Wizara ya Madini imepanga kununua mitambo 15 ya uchorongaji wa miamba kwa ajili ya utafiti wa kina wa madini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita…(endelea).

Hayo yamebainishwa leo tarehe 25 Septemba 25 2023 na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde wakati akizungumza katika kipindi cha Jambo Tanzania (TBC1) kwenye maonesho  ya sita ya teknolojia ya madini yanayoendelea katika viwanja vya EPZ bomba mbili mkoani Geita.


Akielezea kuhusu mkakati wa  VISION 2030 Madini ni Maisha na Utajiri, Mavunde  amesema kuwa Serikali imejipanga kufanya utafiti wa Madini nchi nzima kwa lengo la kupata taarifa zitakazo weza kufungamanisha sekta ya madini na sekta nyingine za kiuchumi.

Akifafanua hali ya utafiti wa madini  amesema mpaka sasa utafiti wa kina umefanyika kwa asilimia 16 tu ambazo taarifa zake ndio zinatumika lengo  la Serikali ni kuongeza taarifa kupitia tafiti nyingine ziitakazofanywa na GST.

Mpaka sasa sekta ya madini inachangia asilimia 56 ya fedha za kigeni ambazo zinachangia asilimia 9.1 ya pato la Taifa(GDP) , hii ni kwa utafiti wa 16% uliofanyika , hivyo kufikia 2030 tutakuwa  tumefanya utafiti nchi nzima.

Sambamba na hapo Mavunde ameeleza kuwa Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira  zitaendeleza juhudi za kutunza mazingira kama Sheria zinavyoelekeza.

Pia Waziri Mavunde ameshiriki zoezi la upandaji miti katika viwanja vya maonesho vya EPZ.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!