Friday , 17 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Mtwara Girls waondokana na changamoto ya maji
ElimuHabari Mchanganyiko

Mtwara Girls waondokana na changamoto ya maji

Spread the love

 

WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Wasichana mkoani Mtwara (Mtwara Girls High School), wameishukuru Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwaondolea changamoto ya uhaba wa maji iliyodumu shuleni hapo kwa muda mrefu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara … (endelea).

Shukrani hizo zimetolewa na wanafunzi hao, baada ya huduma ya maji ya uhakika kurejea shuleni hapo kufuatia hatua ya Rais Samia kuzindua chujio la maji katika mradi wa Mangamba.

Sekondari ya Mtwara Girls ni miongoni mwa wanufaika wa mradi huo uliozinduliwa rasmi na Rais Samia katika ziara yake ya kikazi kwenye mikoa ya kusini, aliyofanya hivi karibuni.

Rais Samia Suluhu Hassan

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake, Farida Twaha amesema “tunafurahia huu mradi mpya uliozinduliwa na Rais Samia, umesaidia kutatua changamoto ya maji iliyokuwepo muda mrefu. Kabla ya mradi kuzinduliwa kulikuwa na changamoto ya maji.”

Farida amesema, upatikanaji wa maji safi na salama utawasaidia kukidhi mahitaji yao ya kila siku, kutokana na watoto wa kike kuwa na uhitaji mkubwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!