Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mgawo wa umeme wang’oa vigogo TANESCO
Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme wang’oa vigogo TANESCO

Spread the love

 

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewahamisha waliokuwa vigogo wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), katika kipindi ambacho kuna changamoto ya ratiba ya upatikanaji nishati hiyo nchini. Anaripoti Matilda Peter, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Zuhra Yunus, imesema leo tarehe 23 Septemba 2023, Rais Samia amemteua Jenerali Paul Kisesa Simuli, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO, akichukua nafasi ya Omar Issa, aliyepangiwa majukumu mengine katika Ofisi ya Rais-Tume ya Mipango.

Kigogo mwingine aliyeondolewa TANESCO ni aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Maharagande Chande, ambaye Rais Samia amemteua kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL).

Rais Samia amemteua Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga, kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO. Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi Nyamo-Hanga aliwahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Mabadiliko hayo yamefanywa na Rais Samia , baada ya wananchi kuibua vilio vyao juu ya changamoto ya kukatika kwa umeme, ikiwemo athari wanazopata kiuchumi.

Akitangaza ratiba ya upatikanaji wa umeme, Chande alidai hatua hiyo inajiri kutokana na upungufu wa uzalishaji wake.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dotto Biteko, alisema serikali inachukua hatua za haraka kutafuta Suluhu ya changamoto hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yatoa kauli wanaolala nje Hospitali ya Muhimbili

Spread the loveSERIKALI imesema inajipanga kushirikiana na sekta binafsi kujenga majengo yatakayosaidia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara yaomba bajeti ya Sh. 67.9 bilioni, wamachinga watengewa bilioni 10

Spread the loveBAJETI ya Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na...

Habari MchanganyikoTangulizi

Migogoro ya ndoa yaongezeka, Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveMIGOGORO ya ndoa na familia imeongezeka kwa asilimia 8.3  kutoka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yahamasisha uanzishaji vituo vya kulea watoto wachanga

Spread the loveSERIKALI imewahimiza wananchi kujenga vituo vya kulelea watoto wadogo na...

error: Content is protected !!