Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Waziri Majaliwa wadhifa wake ni mkubwa
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia: Waziri Majaliwa wadhifa wake ni mkubwa

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake lazima imuenzi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kwa kutekeleza miradi ya maendeleo katika jimbo lake la Ruangwa, ili kuenzi mchango wake katika kulitumikia taifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Lindi … (endelea).

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Ruangwa Mjini, mkoani Lindi, leo tarehe 18 Septemba 2023, Rais Samia amesema Majaliwa wadhifa wake ni mkubwa hivyo lazima atunzwe.

“Wana Ruangwa mmesema maendeleo ni mengi na mengi yako njiani yanakuja. Waswahili wanasema mcheza kwao hutunzwa, kwa nini tusimtunze waziri mkuu kwa maendeleo. Lazima Serikali tumtunze kwa maendeleo. Wadhifa wake ni mkubwa, kazi yake ni kubwa ya kushughulikia Tanzania nzima lazima tumuangalie nyumbani kunakaa sawasawa lazima tulete maendeleo Ruangwa,” amesema Rais Samia.

Mbali na kufikisha maendeleo Ruangwa ili kumuenzi Waziri Majaliwa, Rais Samia amesema Serikali itaendelea kupeleka fedha za maendeleo mkoani Lindi, ili kuifungua kiuchumi huku akiahidi kutumia rasilimali zilizopo katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Rais Samia amesema, kwa mwaka wa fedha uliopo Serikali yake imetenga fedha kiasi cha Sh. 77 bilioni, kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Aidha, Rais Samia amesema Serikali itafanya tathmini ili kujua kiwango cha madini yaliyoko Lindi, ili itafute wawekezaji pamoja na kuandaa namna bora itakayowezesha wachimbaji wadogo kuchimba hasa madini ya dhahabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!