Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wadau wataja tamu, chungu utekelezaji maendeleo endelevu
Habari Mchanganyiko

Wadau wataja tamu, chungu utekelezaji maendeleo endelevu

Spread the love

 

WAKATI Serikali ya Tanzania ikiongeza juhudi katika utekelezaji wa Malengo Endelevu ya Maendeleo (SDG’s), ombwe la umasikini kati ya wananchi wa mijini na vijijini, limetajwa kukwamisha jitihada hizo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 14 Septemba 2023 na Muungano wa Asasi za Kiraia Zinazopambana na Umasikini Tanzania (GCAP Tanzania Coalition), wakati ukitoa tathimini yake juu ya mafanikio na changamoto zilizopatikana katika utekelezaji wa nusu muhula wa SDG’s, unaotarajiwa kufika tamati 2030.

Akizungumza wakati anatoa tathimini hiyo, Mratibu wa GCAP, Martina Kabisana, amesema umaskini umeendelea kuongezeka katika maeneo ya vijijini, kutokana na mamlaka kutoweka usawa katika ugawaji rasilimali fedha, pamoja na kufikisha miradi ya maendeleo.

“Licha ya hatua za maendeleo tulizopiga, umasikini umeendelea kuongezeka kwa kasi hasa kwa pengo kati ya watu wa vijijini na mijini kiuchumi kuongezeka, kukosekana kwa usawa wa kipato na ukosefu wa usawa wa huduma za jamii hasa vijijini na mijini bado changamoto,” amesema Kabisama.

Ametaja changamoto nyingine zilizoibuka katika utekelezaji wa SDG’s, ikiwemo kusuasua kwa utawala bora, uwazi na uwajibikaji na uharibifu wa mazingira.

“Tunashauri Serikali na wadau waongeze juhudi kupunguza pengo la umaskini mijini na vijijini na kuhakikisha kuwa hakuna atakayeachwa nyuma. Kuimarisha utawala bora, uwazi na uwajibikaji katika ngazi zote ili kuhakikisha ugawaji wa rasilimali za umma na utoaji huduma unakuwa wa ufanisi na usawa,” amesema Kabisana.

Alisema kutokana na changamoto hizo, GCAP itatumia wiki ya hamasa ulimwenguni juu ya utekelezaji malengo hayo 17, yaliyowekwa kwa ajili ya kuondoa umasikini.

Katika hatua nyingine, Kabisama ametaja mafanikio yaliyopatikana kwenye utekelezaji wa SDG’s, ikiwa pamoja na ongezeko la uandikishaji wanafunzi katika shule za msingi na sekondari, lililotokana na uamuzi wa Serikali kutoa elimu bure.

Mafanikio mengine ni kuongezeka kwa kasi ya ukuaji uchumi na kupeleka Tanzania kuingia katika kundi la nchi zenye uchumi wa kati 2019 na kuimarika kwa usawa wa kijinsia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!