Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu afufua matukio ya wasiojulikana, ambana Rais Samia
Habari za SiasaTangulizi

Lissu afufua matukio ya wasiojulikana, ambana Rais Samia

Spread the love

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (Chadema) Bara, Tundu Lissu, amedai bila ya wahanga wa vitendo vya watu wasiojulikana kupatiwa haki zao, falsafa ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuhusu upatanisho, haitawezekana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara…(endelea).

Lissu ametoa kauli hiyo leo tarehe 7 Septemba 2023, katika mkutano wa hadhara  uliofanyika Kata ya Issenye mkoani Mara, wakati akikumbushia miaka sita tangu alipojeruhiwa kwa risasi na watu wasiojulikana, jijini Dodoma.

“Watu walioumizwa kipindi hicho kwa namna mbalimbali ni wengi sana, wapo waliopoteza ndugu zao wanadai majibu kwa nini ndugu zao waliuawa, wapo waliopotezwa miaka mitano sasa haijulikana wamepelekwa wapi na ndugu zao wanataka wajue waliowapoteza wapo wapi,” amesema Lissu.

Mwanasiasa huyo amesema “rais wetu anazungumzia upatanishi, hakuna upatanishi bila ukweli, bila kutuambia nani aliyekosa na kwa nini alikosa, aliyekosew anarekebishwaje. Upatanishi sio maneno lazima uendane na vitendo. Ili kupata upatanishi lazima waliotyukosea wajulikane, watubu dhambi na waliosewa wafutwe machozi yao.”

Akizungumzia tukio la kushambuliwa kwa risasi na wasiojulikana lililotokea tarehe kama ya leo 2017, Lissu amemhoji Rais Samia na Mkuu mpya wa Jeshi la Polisi (IGP), Camillius Wambura, wana mpango gani wa kuwachukulia hatua waliolitekeleza.

“Rais Samia alikuwa makamu wa Rais wakati ule na sasa ni rais, atuambie nani aliyekuja kuniua tarehe kama ya leo miaka sita iliyopita na ana mpango gani wa kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria aliyoapa kuilinda na kuitekeleza,” amesema Lissu na kuongeza:

“La pili aniambie angalau ana mpango gani kwa sababu niliumizwa nikiwa bungeni na mbunge ana haki ya kutibiwa kwa gharama ya serikali. Mama aniambie ana mpango gani kama upo wa kulipa stahili zote za matibabu kwa mujibu wa sheria.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!